Apr 27, 2024 02:47
Wahudumu wa afya, timu za uokoaji na mashirika ya kutetea haki za binadamu yanawashutumu askari vamizi wa jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kuwanyofoa viungo Wapalestina na hata kuwazika baadhi yao wakiwa hai kwenye makaburi ya halaiki yaliyogunguliwa kwenye eneo la karibu na Hospitali ya Nasser huko Ukanda wa Ghaza, baada ya askari hao katili kuondoka katika eneo hilo Aprili 7 kufuatia mashambulizi ya ardhini ya miezi minne.