-
Raia 102 wa kigeni magaidi na matapeli wa mitandaoni watimuliwa Nigeria, wengi wao ni Wachina
Aug 22, 2025 06:34Serikali ya Nigeria imewatimua raia wa kigeni 102 wakiwemo Wachina 50 waliopatikana na hatia ya kuhusika na "ugaidi wa mitandaoni na utapeli wa mitandaoni".
-
Jeshi la Sudan lakanusha kushambulia msafara wa misaada wa WFP katika jimbo la Darfur
Aug 22, 2025 06:33Jeshi la Sudan (SAF) limekanusha madai yaliyotolewa wapiganaji wa Vikosi vya Usaidzi wa Haraka (RSF) kuwa limefanya mashambulizi ya angani dhidi ya msafara wa misaada wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) uliokuwa unapeleka misaada Darfur.
-
Wabunge wa Kenya wamtaka Rais Ruto awasilishe mahakamani ushahidi wa wabunge kula hongo
Aug 22, 2025 04:01Uongozi wa Bunge la Kitaifa la Kenya umepuuza matamshi yaliyotolewa na Rais William Ruto kuhusu madai ya hongo bungeni, ukisema ni tuhuma tupu, na kumtaka atoe ushahidi wa madai hayo ya ufisadi.
-
Jibu la Tunisia kwa kauli ya Netanyahu ni ishara ya wasiwasi wa nchi za Kiarabu kuhusu mipango ya upanuzi ya Israel
Aug 21, 2025 22:43Wananchi wa Tunisia wamefanya maandamano ya kupinga uzayuni wakilaani matamshi ya Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, Benjamin Netanyahu, kuhusu kile kinachoitwa “Israeli Kubwa.”
-
Amnesty International: Haki za binadamu zimekiukwa mashariki mwa Kongo
Aug 21, 2025 22:42Shirika la Msamaha Duniani, Amnesty International, limezituhumu pande zinazozozana mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwa kufanya ukiukwaji wa kutisha wa haki za binadamu ikiwa ni pamoja na vitendo vya kubaka kwa umati, mauaji ya kiholela na utekaji nyara.
-
Human Rights Watch yakosoa kitendo cha Burkina Faso kumfukuza afisa wa UN
Aug 21, 2025 08:13Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limekosoa uamuzi wa serikali ya kijeshi ya Burkina Faso kumfukuza mwakilishi wa Umoja wa Mataifa, Carol Flore-Smereczniak, na kumtangaza kuwa "mtu asiyetakikana," nchini humo na kutoa wito kwa mamlaka ya kijeshi kushirikiana na Umoja wa Mataifa badala ya "kuficha ukiukwaji wa haki za binadamu."
-
Makubaliano ya amani ya DRC: Maeneo yanayodhibitiwa na M23 kurejeshwa mikononi mwa serikali
Aug 21, 2025 06:24Makubaliano ya amani yaliyopendekezwa kati ya serikali ya Congo na waasi wa M23 wanaodaiwa kuuungwa mkono na Rwanda yanataka kurejesha udhibiti wa serikali katika maeneo yanayodhibitiwa na waasi.
-
Makumi waaga dunia kwa mafuriko nchini Niger, maelfu waathirika
Aug 21, 2025 02:12Kwa uchache watu 47 wamepoteza maisha, huku zaidi ya 56,000 wakilazimika kuhama makazi yao kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa zilizonyesha hivi majuzi nchini Niger.
-
Amnesty yaikosoa Nigeria kwa kuwakandamiza Waislamu wakiitetea Gaza
Aug 21, 2025 01:43Mkurugenzi wa shirika la kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International nchini Nigeria, Isa Sunusi, amelaani vikali ukandamizaji mkali wa vyombo vya serikali dhidi ya Waislamu wa madhehebu ya Shia, wakati wa maandamano ya kulaani jinai za Israel dhidi ya Wapalestina wa Gaza, na kusema kuwa takriban wanachama 83 wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria bado wako rumande bila kufunguliwa mashtaka, licha ya kupata majeraha ya risasi na makovu mengineo wakishiriki maandamano ya amani.
-
Waziri wa Mambo ya Ndani wa Sudan: Tunafanya kazi kwa bidii kudhibiti usalama na uwepo wa kigeni nchini
Aug 21, 2025 08:14Waziri wa Mambo ya Ndani wa Sudan, Luteni Jenerali Babiker Samra amesema kwamba uwepo haramu wa wapiganaji wa kigeni nchini humo hauwezi tena kuvumiliwa, kutokana na athari zake mbaya za kiusalama, kiuchumi na kijamii.