-
Umoja wa Mataifa: Maafisa wetu wamezuiwa na M23 kuingia mashariki ya Congo
Jul 24, 2025 23:08Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, wataalamu wake walizuiwa na waasi wa M23 kufanya uchunguzi wao katika ngome wanazoshikilia mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC).
-
Mlipuko wa kipindupindu wauwa watu 13 katika jimbo la Niger, nchini Nigeria
Jul 24, 2025 07:01Takriban watu 13 wamefariki dunia na wengine 239 wameambukizwa ugonjwa wa kipindupindu unaoendelea kuenea katika wilaya sita za jimbo la Niger katikati mwa Nigeria. Taarifa hii imetolewa na mamlaka husika katika jimbo la Niger.
-
Maisha ya watu milioni 1.3 Nigeria yako hatarini baada ya WFP kusitisha misaada
Jul 24, 2025 03:19Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limetangaza kuwa litalazimika kusitisha msaada wa chakula na lishe kwa watu milioni 1.3 katika eneo lililokumbwa na machafuko zaidi kaskazini mashariki mwa Nigeria mwishoni mwa mwezi huu wa Julai kutokana na hifadhi yake ya chakula na virutubisho vya lieshe kumalizika.
-
Sheikh Mkuu wa al-Azhar atoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka kuiokoa Gaza
Jul 23, 2025 23:19Sheikh Mkuu wa al-Azhar ya Misri ametoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka na jamii ya kimataifa kuokoa maisha ya wakaazi wa Ukanda wa Gaza kutokana na kifo cha njaa.
-
Kaunti za Busia, Bungoma na Kakamega nchini Kenya zathibitisha maambukizo ya ugonjwa wa Mpox
Jul 23, 2025 08:37Magharibi mwa Kenya sasa ndio kitovu cha mlipuko wa ugonjwa wa Mpox huku kaunti za Busia, Bungoma na Kakamega nchini humo zikithibitisha kuwa na wagonjwa kadhaa walioambukizwa ugonjwa huo unaosababishwa na virusi.
-
Russia na Msumbiji zathibitisha tena ushirikiano wa kiulinzi baada ya mkutano wa mawaziri wa mambo ya nje
Jul 23, 2025 07:26Russia na Msumbiji zimetihibitisha kwa mara nyingine ushirikiano wa kiulinzi kati ya nchi mbili hizo kufuatia ziara ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Msumbiji mjini Moscow.
-
Ufaransa yasisitiza uwakilishi zaidi wa nchi za Kiafrika katika Baraza la Usalama la UN
Jul 23, 2025 07:21Mwakilishi wa Ufaransa katika Umoja wa Mataifa ameeleza kuwa Paris inaunga mkono kufanyika mageuzi katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa (UNSC) ili kuongeza uwakilishi wa mataifa ya Afrika katika taasisi hiyo ya kimataifa.
-
Katika wiki moja vifo 18, maambukizi 1,300 ya kipindupindu yaripotiwa Sudan iliyogubikwa na vita
Jul 23, 2025 02:42Wizara ya Afya ya Sudan imeripoti maambukizi mapya ya kipindupindu, huku idadi hiyo ikifika 1,307 na vifo 18 vilivyosababishwa na ugonjwa huo ndani ya muda wa wiki moja.
-
Raila Odinga: Sikufaidika na hendisheki ya Uhuru Kenyatta
Jul 23, 2025 00:11Kiongozi wa chama cha ODM nchini Kenya, Bwana Raila Odinga amepuuza madai yanayosema kuwa alinufaika kutokana na ushirikiano kati yake na Rais Mstaafu, Uhuru Kenyatta, akisema hakupewa nafasi yoyote serikalini au kupata manufaa ya kibinafsi.
-
Wagombea 81 wachukua fomu ya kuwania kiti cha urais Cameroon
Jul 22, 2025 10:39Jumla ya wagombea 81 wamejaza fomu na kuwasilisha kwa Tume ta Taifa ya Uchaguzi ya nchi hiyo kwa ajili ya kushiriki katika uchaguzi wa Rais wa Oktoba mwaka huu.