-
Zakzaky: Mipango ya kuwafukuza Wapalestina Gaza, kuipokonya silaha Hizbullah itafeli
Aug 19, 2025 07:14Kiongozi wa Harakati ya Kiislamu ya Nigeria, Sheikh Ibrahim Yaqoub Zakzaky amebainisha kuwa, mipango ya utawala wa Kizayuni ya kuwaondoa kwa nguvu Wapalestina wa Ukanda wa Gaza katika ardhi yao na kuipokonya silaha Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon kwa kutumia serikali ya Beirut itagonga mwamba.
-
Watu 52 wauawa kwa kupigwa mapanga na waasi wa ADF mashariki ya Kongo, DR
Aug 19, 2025 03:05Maafisa wa Umoja wa Mataifa na wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, DRC wamesema, katika siku za karibuni, waasi wa Allied Democratic Forces, ADF waliokuwa na mapanga wamewaua raia wapatao 52 katika maeneo ya Beni na Lubero mashariki mwa nchi hiyo.
-
Matumaini ya kupatikana suluhisho la kisiasa baina ya serikali ya Kongo DR na M23 yaongezeka
Aug 18, 2025 23:34Matarajio ya kufikiwa suluhisho la amani nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo yameongeka baada ya miongo kadhaa ya vita vya kikatili mashariki mwa nchi hiyo.
-
Jeshi la Sudan latuhumiwa kuwatesa watu hadi kufa
Aug 18, 2025 07:42Shirika maarufu la kutetea haki za binadamu nchini Sudan limelishutumu jeshi la nchi hiyo na vikosi vya usalama kwa kuwatesa watu hadi kuwaua pamoja na kuwa na "vyumba vya kufanya mauaji".
-
ADF yanyooshewa kidole cha lawama kwa mauaji mapya ya Kivu Kaskazini
Aug 18, 2025 05:01Waasi wa ADF wameongeza mashambulizi dhidi ya raia katika siku za hivi karibuni mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Jumapili ya jana, Agosti 17, watu wasiopungua tisa waliuawa katika mji wa Oicha, makao makuu ya eneo la Beni, kulingana na vyanzo vya afya na utawala vya eneo hilo.
-
Maandamano ya kutaka kulindwa wanahabari wa Gaza yafanyika Afrika Kusini
Aug 18, 2025 03:18Waandishi wa habari wa Afrika Kusini na wafanyakazi wa vyombo vya habari wameongoza maandamano huko Sea Point jijini Cape Town, wakishinikiza kupewa ulinzi zaidi waandishi wa habari wa Palestina huko Gaza, sanjari na kutangaza mshikamano na wenzao waliouawa katika ukanda huo wa Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
-
Qatar: Tumezikabidhi DRC, M23 rasimu ya makubaliano ya amani
Aug 18, 2025 03:14Qatar imetangaza habari ya kukabidhi rasimu ya makubaliano ya amani kwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kundi la waasi la M23, ikiwa ni sehemu ya mchakato wa amani unaoendelea Doha, vyombo vya habari vya DRC viliripoti hayo jana Jumapili, vikimnukuu afisa wa Qatar.
-
Wanahabari Nigeria walaani mauaji ya waandishi wenzao huko Gaza
Aug 18, 2025 03:13Muungano wa Waandishi wa Habari wa Nigeria (NUJ) umelaani vikali mauaji ya wanahabari yaliyofanywa na utawala ghasibu wa Israel huko Gaza na kusisitiza kuwa, hujuma hizo za utawala wa Kizayuni dhidi ya waandishi wenzao katu haziwezi kuwazuia wahudumu wa tasnia hiyo kuendelea kufichua ukweli.
-
Madaktari wa Sudan: RSF imeua watu wengi kwenye kambi ya Abu Shouk, wamo watoto saba
Aug 17, 2025 23:56Mtandao wa Madaktari wa Sudan umeripoti kuwa, wapiganaji wa Vikosi vya Usaidizi wa Haraka (RSF) wamefyatua makombora kwenye kambi ya wakimbizi waliokumbwa na njaa katika eneo la magharibi mwa Darfur na kusababisha vifo vya watu wasiopungua 31 wakiwemo watoto saba na mwanamke mjamzito.
-
DRC yapinga kupelekwa balozi mdogo wa Kenya mjini Goma
Aug 17, 2025 08:07Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imepinga hatua ya Kenya ya kumteua balozi mdogo anayetazamiwa kutumwa katika mji wa Goma ulioko mashariki mwa DRC, ikiuelezea uamuzi huo kuwa "usiofaa".