-
Mashindano ya Kimataifa ya Qur'ani Yafunguliwa Algeria
Jan 22, 2025 10:03Mashindano ya 20 ya Kimataifa ya Kuhifadhi na Kusoma Qur'ani ya Algeria yamefunguliwa huko Algiers, mji mkuu wa Algeria.
-
UN: Mapambano dhidi ya ugaidi barani Afrika yaheshimu haki za binadamu
Jan 22, 2025 10:03Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, mapambano ya kukabiliana kikamilifu na ugaidi barani Afrika yanapaswa kuhusisha uvumbuzi na mtazamo unaoheshimu haki za binadamu na utawala wa sheria.
-
Kenya yarahisisha masharti ya safari kwa karibu nchi zote Afrika
Jan 22, 2025 09:49Kenya imetangaza kuwa, itawaruhusu raia wa karibu mataifa yote ya Afrika kuzuru nchini humo bila kuhitaji idhini ya awali. Hiyo ni kulingana na agizo jipya la baraza la mawaziri la nchi hiyo ya Afrika Mashariki.
-
IGAD: Mataifa ya Pembe ya Afrika kushuhudia kiwango kidogo cha mvua
Jan 22, 2025 09:49Kitengo cha hali ya hewa cha Jumuiya ya Maendeleo ya Kiserikali (IGAD) kimesema kuwa, eneo la Pembe ya Afrika litashuhudia kiwango kidogo cha mvua kuliko kawaida kati ya mwezi Machi na Mei mwaka huu. Ripoti hiyo inatolewa huku Ukanda huo ukiendelea, kukabiliwa na athari za mabadiliko ya tabia nchi.
-
Burkina Faso, Niger na Mali kuunda kikosi cha wanajeshi 5,000 kupambana na waasi
Jan 22, 2025 09:48Nchi tatu zinazotawaliwa na wanajeshi katika kanda ya Sahel Afrika zimetangaza kuunda kikosi cha wanajeshi 5,000 kupambana na ghasia na harakati za makundi ya waasi ambazo zimeyakumba mataifa hayo kwa miaka kadhaa.
-
Africa CDC yazindua kampeni ya haraka baada ya kuthibitishwa kuingia virusi vya Marburg nchini Tanzania
Jan 22, 2025 03:07Kituo cha Afrika cha Kudhibiti na Kuzuia Magonjwa barani Afrika (Africa CDC) kimetangaza mipango ya kuhamasisha msaada wa haraka wa kuisaidia Tanzania kukabiliana na mripuko wa virusi vya Marburg.
-
Ajira 40,000 zimebuniwa katika sekta ya biashara ya Kenya ya kutoa huduma nje
Jan 22, 2025 03:07Sekta ya Biashara ya Kenya (BPO) imefanikiwa kubuni zaidi ya ajira 40,000 hivi karibuni, ikisaidiwa na kuingia wawekezaji wapya waliovutiwa na sera wezeshi na mazingira ya udhibiti.
-
Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo lataka wananchi wawe watulivu, waasi wasonga mbele
Jan 22, 2025 03:06Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) jana Jumanne lilitoa mwito kwa raia kuwa watulivu kutokana na kusonga mbele waasi wa M23 hivi karibuni katika jimbo la Kivu Kaskazini la mashariki mwa nchi hiyo.
-
Wahamiaji 20 wa Ethiopia wafa maji baada ya mashua yao kupinduka nchini Yemen
Jan 22, 2025 03:06Shirika la Kimataifa la Uhamiaji (IOM) limetangaza kuwa, wahamiaji 20 wa Ethiopia, wakiwemo wanawake tisa na wanaume 11, wamekufa maji wakati mashua yao ilipopinduka katika pwani ya kusini mwa Yemen, mwishoni mwa juma.
-
Waasi wa M23 wauteka mji wa kistratajia mashariki mwa DRC
Jan 21, 2025 23:19Waasi wa M23 wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wameuteka mji wa mashariki wa Minova, njia kuu ya usambazaji wa bidhaa huko Goma, makao makuu ya mkoa wa Kivu Kaskazini.