-
Rais Tshisekedi: Mazungumzo ya amani na waasi wa M23 yataanza tena Doha
Nov 03, 2025 03:02Rais Felix Tshisekedi wa DRC amesema kuwa, mazungumzo ya amani kati ya serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) na kundi la waasi la Machi 23 (M23) yataanza tena wiki ijayo huko Doha, mji mkuu wa Qatar.
-
Wasudan 177,000 wamekwama katika mji ulioteketea
Nov 02, 2025 22:53Mji wa El Fasher, ambao ni makao makuu ya jimbo la Darfur Kaskazini nchini Sudan, hatimaye ulitekwa na Vikosi vya Msaada wa Haraka RSF hivi karibuni baada ya kuzingirwa kwa muda wa miezi 18 na hivi sasa ripoti zinasema kuwa Wasudan 177,000 wamekwama kwenye mji huo.
-
Wahamiaji 45 wasio na vibali waokolewa pwani ya mashariki ya Libya
Nov 02, 2025 22:51Wahamiaji 45 wasio na vibali wameokolewa kwenye pwani ya mji wa Tobruk wa mashariki mwa Libya. Hayo ni kwa mujibu wa gazeti la Libya Al-Watan ambalo limesema kuwa wahamiaji hao wamekabidhiwa kwa mamlaka husika baada ya kufanyiwa uchunguzi wa kimatibabu.
-
Umoja wa Afrika wampongeza Samia Suluhu Hassan kwa kuchaguliwa kuiongoza Tanzania
Nov 02, 2025 07:58Umoja wa Afrika umempongeza Samia Suluhu Hassan kwa kuchaguliwa kuingoza Tanazania kwa muhula mwigine baada ya kuibuka na ushindi katika uchaguzi mkuu uliofanyika tarehe 29 mwezi uliopita wa Oktoba.
-
Rais Pezeshkian aipongeza Algeria kwa maadhimisho ya Siku ya Uhuru
Nov 02, 2025 07:14Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa pongezi za dhati kwa Rais na watu wa Algeria kwa mnasaba wa maadhimisho ya miaka 71 ya kuanza Mapinduzi ya Ukombozi na Siku ya Taifa ya Algeria na kusema: Uhusiano wa kihistoria kati ya Iran na Algeria unafungua njia ya kupanuliwa zaidi uhusiano kati ya nchi hizo mbili.
-
Nigeria yapinga vikali vitisho vya Trump, yasema mamlaka yake ya kujitawala hayajadiliwi
Nov 02, 2025 07:11Serikali ya Nigeria imepinga vikali uingiliaji wowote wa kigeni katika mambo ya ndani ya nchi hiyo ikisisitiza kwamba "mamlaka ya kitaifa hayawezi kujadiliwa," na kwamba inachunguza matukio ya hivi karibuni na kuwafuatilia wale wote waliohusika.
-
Trump atishia kuishambulia kijeshi Nigeria kwa tuhuma za alichokiita 'kuuliwa raia Wakristo wapendwa'
Nov 02, 2025 02:56Rais Donald Trump wa Marekani ametishia kufanya mashambulizi ya kijeshi ndani ya ardhi ya Nigeria kutoa mjibizo kwa alichodai kuwa ni ukatili wanaofanyiwa Wakristo, akisema ameiagiza Wizara yake ya Vita aliyoipa jina hilo jipya hivi karibuni "kujiandaa kwa hatua zinazowezekana" kuchukuliwa.
-
Watu 21 wameaga dunia na 30 hawajulikani walipo kufuatia maporomoko ya udongo yaliyoikumba Kenya
Nov 01, 2025 23:44Maporomoko ya udongo yaliyoathiri maeneo ya magharibi mwa Kenya yameuwa watu wasiopungua 21 na kujeruhi makumi ya wengine. Watu wengine zaidi ya 30 hawajulikani walipo kufuatia maafa hayo.
-
Komoro kujiunga na kesi ya mauaji ya kimbari dhidi ya Israel katika Mahakama ya ICJ
Nov 01, 2025 23:42Komoro imewasilisha tamko rasmi la kujiunga na kesi ya mauaji ya kimbari dhidi ya Israel iliyofunguliwa na Afrika Kusini katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ).
-
RSF yawatia mbaroni wanamgambo wake wanaotuhumiwa kufanya jinai el Fasher Sudan
Nov 01, 2025 08:11Vikosi vya Msaa wa Haraka RSF nchini Sudan vimetangaza kuwa vimewatia mbaroni wapiganaji wanaoshutumiwa kukiuka haki za binadamu na kufanya mauaji ya umati kwenye mji wa El-Fasher uliotekwa na kundi hilo hivi karibuni.