-
Mapigano yashadidi DRC, kila upande unamtuhumu mwenzake
Dec 03, 2025 03:05Mapigano yamezidi kupamba moto mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo huku jeshi na waasi wa M23 kila upande ukimshutumu mwenzake kwa kukanyaga makubaliano ya kusitisha mapigano.
-
UNHCR: Watu 100,000 wamekimbia Kaskazini mwa Msumbiji huku machafuko yakishadidi
Dec 02, 2025 23:18Watu takribani 100,000 wamelazimika kuyakimbia makazi yao kaskazini mwa Msumbiji ndani ya wiki mbili pekee. Hayo ni kwa mujibu wa taarifa ya Jumanne ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR, ambalo limeonya juu ya mashambulizi kuongezeka na kuyakumba maeneo ambayo hapo awali yalikuwa salama, na hivyo kuongeza mzigo wa wahudumu wa kibinadamu waliokwisha elemewa.
-
Wakuu wa ECOWAS wazuru Guinea-Bissau baada ya mapinduzi ya kijeshi
Dec 02, 2025 23:08Ujumbe wa upatanishi wa ngazi ya juu kutoka Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS) ulifanya mkutano Jumatatu na viongozi wa mpito wa Guinea-Bissau kujadili njia ya amani ya kumaliza mgogoro wa kisiasa uliosababishwa na mapinduzi ya kijeshi ya wiki iliyopita.
-
Rais Samia: Vurugu za uchaguzi zililenga kuiangusha serikali
Dec 02, 2025 09:54Rais Samia Suluhu Hassan wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amefichua kuwa vurugu za uchaguzi wa Oktoba 29 ziliratibiwa na watu wa ndani na nje ya nchi kwa lengo la kuibomoa serikali, na kuzionya vikali taasisi za dini.
-
Sakata la usalama, Waziri wa Ulinzi wa Nigeria ajiuzulu
Dec 02, 2025 09:50Waziri wa Ulinzi wa Nigeria, Mohammed Badaru Abubakar amejiuzulu, katika kipindi ambacho nchi hiyo inakabiliwa na mgogoro wa usalama unaojumuisha utekaji nyara wa watoto wa shule kwa wingi.
-
Viongozi wa Afrika watoa wito wa kutambuliwa rasmi uhalifu wa enzi za ukoloni na kulipwa fidia
Dec 02, 2025 02:55Viongozi wa Afrika waliokutana Algiers siku ya Jumapili walitoa wito wa kutambuliwa rasmi uhalifu uliofanyika enzi za ukoloni barani Afrika, ufanywe kuwa ni uhalifu na kulipwe fidia kupitia mchakato unaoungwa mkono na Umoja wa Afrika.
-
Mshindi wa Tuzo ya Nobel, Denis Mukwege: Makubaliano ya amani kati ya Kinshasa na M23 ni 'haramu'
Dec 02, 2025 02:53Mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Dkt. Denis Mukwege amelaani mchakato wa amani unaoendelea kati ya serikali ya Kinshasa na waasi wa M23 unaolenga kukomesha mapigano mashariki mwa DRC.
-
UN yatahadharisha kuhusu janga la njaa linalotishia wakimbizi nchini Ethiopia
Dec 01, 2025 23:12Shirika la Mpango wa Chakula Duniani la Umoja wa Mataifa (WFP) limeonya kwamba wakimbizi nchini Ethiopia wako katika hatari ya kufa njaa kutokana na uhaba mkubwa wa fedha unaolilazimisha shirika hilo kupunguza mgao wa chakula.
-
Cameroon: Mpinzani wa Rais Biya amefariki dunia akiwa kizuizini
Dec 01, 2025 11:13Kiongozi wa kisiasa na kinara wa chama cha upinzani cha Manidem nchini Cameroon, Anicet Ekane, amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Jumatatu, Desemba 1.
-
Ethiopia yazindua mkakati wa miaka mitano wa kuendeleza uchumi wa kidijitali
Dec 01, 2025 06:55Serikali ya Ethiopia imezindua Mkakati wa Kidijitali wa Ethiopia 2030, unaolenga kukuza matumizi ya teknolojia katika sekta zote za kiuchumi na kuugeuza uchumi wa nchi hiyo ya Pembe ya kuwa wa kidijitali kikamilifu.