-
Upinzani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati: Hatutashiriki uchaguzi mkuu wa Desemba 28
Oct 09, 2025 07:07Upinzani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati umetangaza kuwa utasusia uchaguzi mkuu uliopangwa kufanyika mwezi Disemba ambapo Rais Faustin-Archange Touadera atawania tena urais kwa muhula wa tatu.
-
Wanaharakati wa Afrika Kusini katika msafara wa Sumud; Tulimkaripia Waziri wa Israel tukiwa kizuizini
Oct 09, 2025 03:44Wanaharakati sita wa Afrika Kusini ambao waliwekwa kizuizini huko Israel baada ya kutekwa nyara kutoka katika msafara wa kimataifa wa meli kwa jina la Global Sumud Flotilla kuelekea Gaza wamesimulia hadithi za kusikitisha kuhusu walichopitia wakiwa mikononi mwa wanajeshi wa Israel.
-
Wanamgambo wa RSF washambulia hospitali jimboni Darfur; watu 12 wameuawa, 17 kujeruhiwa
Oct 09, 2025 03:44Raia wasiopungua 12 wameuawa na wengine 17 kujeruhiwa katika shambulio lililofanywa na wanamgambo wa Kikosi cha Msaada wa Haraka (RSF) katika jimbo la Darfur Kaskazini.
-
Rais wa Madagascar afanya mazungumzo licha ya waandamanaji kususia
Oct 09, 2025 03:43Rais Andry Rajoelina wa Madagascar jana aliyaalika makundi na asasi kadhaa za kiraia kwa ajili ya mazungumzo katika ikuu ya Rais.
-
Ethiopia yaituhumu Eritrea kuwa inajiandaa kuanzisha vita dhidi yake
Oct 09, 2025 03:43Ethiopia imeituhumu Eritrea kuwa inajiandaa kuanzisha vita dhidi yake. Ethiopia imetoa tuhuma hizi dhidi ya Eritrea ikiwa ni ishara ya karibuni ya kushtadi mvutano katika nchi mbili hizo jirani kuhusu udhibiti wa Bahari Nyekundu.
-
ICRC: Mgogoro wa afya Kongo DR unazidi kuwa mbaya
Oct 08, 2025 23:41Mfumo wa huduma za afya katika eneo linalokumbwa na migogoro mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) umezorota kwa kiasi kikubwa, huku vituo vingi vya matibabu vikiwa na uhaba mkubwa wa dawa na wafanyakazi, Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC) imeonya katika taarifa yake ya jana Jumatano.
-
Somalia yakanusha vikali kufikia makubaliano ya siri na Sweden kuhusu kuwarejesha nchini raia wake
Oct 08, 2025 08:58Ofisi ya Waziri Mkuu wa Somalia leo imetoa taarifa na kukadhibisha vikali Somalia kwamba imefikia makubaliano ya siri na Sweden kuhusu kuwarejesha nyumbani raia wa Somalia kutoka Sweden ukiwemo pia mpango wa msaada wenye masharti kwa Somalia.
-
Rais wa Madagascar kufanya mazungumzo ya kitaifa leo
Oct 08, 2025 03:06Rais Andry Rajoelina wa Madagascar amesema anapanga kufanya "mazungumzo ya kitaifa" na makundi mbalimbali leo Jumatano baada ya vijana waandamanaji kutoa makataa ya saa 48 ili akubali matakwa yao la sivyo akabiliwe na maandamano ya kitaifa.
-
Umoja wa Mataifa waeleza wasiwasi kuhusu machafuko kaskazini mwa Msumbiji
Oct 08, 2025 03:05Umoja wa Mataifa umeelezea wasiwasi ulionao kuhusu idadi kubwa ya raia wanaokimbia machafuko yanayoendelea kaskazini mwa Msumbiji, ambapo wengi wao wamefikia hatua ya kukata tamaa.
-
Mazungumzo ya waasi wa M23 na serikali ya Kinshasa katika hatihati
Oct 07, 2025 23:12Wakati mapigano yakiripotiwa kuendelea katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kumeibuka swali iwapo awamu ya sita ya mazunguumzo kati ya kundi waasi AFC/M23 na serikali ya Kinshasa yatafanyia juma hili jijini Doha kama ilivyotangazwa na mpatanishi nchi ya Qatar au la.