-
Ali Larijani, Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran, ameuawa Shahidi
Mar 18, 2026 03:43Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran limetangaza kuuawa shahidi kwa katibu wake, Ali Larijani, kufuatia shambulio la maadui, ambao ni Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Araqchi amwambia Guterres: Simamisheni uchokozi wa Marekani na Israel dhidi ya Iran
Mar 17, 2026 08:43Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema: "Matatizo ya usafirishaji wa meli katika Mlango-Bahari wa Hormuz ni matokeo ya vita vilivyoanzishwa na Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel, na kila nchi au shirika la kimataifa linalojali amani na usalama lazima lilaani uhalifu wa tawala hizo mbili na kutoa wito wa kukomeshwa uchokozi wao wa kijeshi dhidi ya taifa la Iran."
-
Araqchi: Vita vitaisha kwa njia itakayomfanya adui asifikirie tena kutushambulia
Mar 17, 2026 07:01Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu haijatuma ujumbe wa aina yoyote kwa wavamizi wala haijaomba kusitishwa vita.
-
Pezeshkian: Iran haitasalimu amri mbele ya madola ya kibeberu
Mar 17, 2026 06:04Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema taifa hili halitasalimu amri kamwe mbele ya madola ya kibeberu, huku akiitaka jamii ya kimataifa kulaani uvamizi wa Marekani na utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Iran yazitaka nchi za Kiislamu zitangaze msimamo, yasema Marekani haiaminiki
Mar 17, 2026 04:45Katika taarifa yenye vipengele sita iliyoelekezwa kwa serikali za nchi za Kiislamu, Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema: “Lazima muamue msimamo wenu katika Vita vya Ramadhani, je, mnasimama upande wa nchi ya Kiislamu ya Iran, au upande wa Marekani na Israel?”
-
Qalibaf: Hali ya Hormuz haitarudi tena kama ilivyokuwa zamani
Mar 17, 2026 04:44Spika wa Majilisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel unalenga kutumia vita kubadilisha muundo wa eneo la Asia ya Magharibi.
-
IRGC: Tumewavurumishia maadui makombora 700, droni 3,600 mpaka sasa
Mar 17, 2026 03:38Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (IRGC) limesema limepiga shabaha za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa makombora zaidi ya 700 na ndege zisizo na rubani 3,600 tangu Jamhuri ya Kiislamu ianzishe operesheni za kulipiza kisasi cha mashambulizi ya kichokozi ya maadui hao mwishoni mwa Februari mwaka huu.
-
Kamanda Naeini: Iran inadhibiti kikamilifu Lango Bahari la Hormuz
Mar 16, 2026 10:31Msemaji wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: Lango Bahari la Hormuz linadhibitiwa kikamilifu na Iran na kwamba uchokokozi wowote utakabiliwa na jibu kali.
-
Araqchi: Kushambulia maghala ya mafuta ni kuangamiza mazingira
Mar 16, 2026 10:28Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa kitendo cha kushambulia maghala ya kuhifadhia mafuta katika mji wa Tehran ni sawa na kuangamiza mazingira.
-
Rais wa Iran amwambia Macron: US, Israel ndio mzizi wa ukosefu wa usalama katika eneo
Mar 16, 2026 06:04Rais wa Iran amesema Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel ndizo chimbuko la ukosefu wa usalama na uthabiti katika eneo la Asia Magharibi, akisisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu haitasita kukabiliana na wavamizi.