-
Iran: Uingiliaji wa Marekani wakusudia kuchochea vurugu na ugaidi
Jan 08, 2026 03:07Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu Iran imekemea vikali kauli za kuingilia na za upotoshaji zilizotolewa na maafisa wa Marekani kuhusu hali za ndani ya Iran, ikisema matamshi hayo yanaakisi uhasama wa kudumu wa Washington dhidi ya taifa hili na yamelenga kuibua machafuko na hali ya kutokuwa na usalama nchini.
-
Meja Jenerali Hatami: Vitisho vya maadui havitapita bila kujibiwa
Jan 07, 2026 11:32Kamanda Mkuu wa Jeshi la Iran, Meja Jenerali Amir Hatami amesema Jamhuri ya Kiislamu inayatazama matamshi ya vitisho na kichochezi ya maadui zake kuwa tishio la moja kwa moja dhidi ya taifa hili, na itatoa majibu madhubiti iwapo vitisho hivyo vitaendelea kutolewa.
-
Baghaei: Israel ibebeshwe dhima kwa mashambulizi ya kinyama Lebanon
Jan 07, 2026 10:20Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetoa wito kwa jamii ya kimataifa kuiwajibisha Israel kwa uhalifu wa kivita, kufuatia wimbi la mashambulizi mabaya dhidi ya Lebanon, na kukanyaga makubaliano ya kusitisha mapigano.
-
Pezeshkian: Maadui wanajaribu kuzuia maendeleo ya taifa kupitia vikwazo
Jan 07, 2026 07:57Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekosoa vikali mashinikizo ya nchi ajinabi dhidi ya taifa la Iran.
-
“Usalama ni Mstari Mwekundu”: Iran yaapa kujibu vikali vitisho vinavyozidi kuongezeka
Jan 07, 2026 02:58Baraza la Ulinzi la Iran limelaani vitisho vinavyozidi kuongezeka, kauli za uchochezi na matamshi ya kuingilia mambo ya ndani, hususan kutoka Marekani, dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, likionya kuwa shambulio lolote dhidi ya usalama, uhuru au mipaka ya ardhi ya taifa litakabiliwa kwa majibu makali.
-
IRGC: Iran haiogopi vitisho na haitakubali kutawaliwa na Marekani
Jan 07, 2026 02:57Naibu Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Brigedia Jenerali Ahmad Vahidi, amesema kuwa Iran haiogopi vitishio vya maadui na kamwe haitakubali kutawaliwa na Marekani. Ametoa kauli hiyo kujibu vitisho vilivyotolewa hivi karibuni na Rais wa Marekani Donald Trump.
-
Qalibaf: Israel ilibembeleza kusitisha mapigano wakati wa vita vya siku 12
Jan 06, 2026 12:11Spika wa Majlisi ya Ushauri wa Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa: Katika siku chache za mwisho za vita vya siku 12, utawala wa Kizayuni uliomba kwa kubembeleza kusitisha mapigano na ukweli huo unaonesha nguvu ya Muqawama wa taifa la Iran mbele ya wavamizi.
-
Baqaei: Vikosi vya Iran viko macho kukabiliana na vitisho vyovyote vya adui
Jan 06, 2026 12:11Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje amesema kuhusu mazingira yaliyozushwa ya kuonesha kuna uwezekano wa kurudiwa uchokozi wa kijeshi dhidi ya Iran na kusisitiza kuwa: Kilicho muhimu na kinachotuhusu sisi ni kuimarisha nguvu zetu na kuwa macho zaidi kulihami taifa la Iran.
-
Iran, Cuba, Brazil zataka kuheshimwa sheria za kimataifa
Jan 06, 2026 06:51Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Cuba na Brazil wamesisitiza udharura wa kuwepo ushirikiano wa karibu na uratibu miongoni mwa nchi zinazostawi katika majukwaa ya kimataifa, ili kukabiliana na mfumo wa ubeberu; na kuunga mkono sheria za kimataifa na kanuni za Hati ya Umoja wa Mataifa.
-
Iran yakanusha uvumi wa vyombo vya habari vya Magharibi kuhusu mazungumzo na Marekani
Jan 06, 2026 03:36Naibu wa Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amekanusha uvunii unaoneshwa na vyombo vya habari vya Magharibi kwamba Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran alifanya mkutano maalumu na waandishi wa habari siku ya Alkhamisi na kuongeza kuwa, inavyoonekana ni kwamba baadhi ya duru za Magharibi zinapenda sana kupata kisingizio cha kusema uongo na kuchochea chuki katika kila jambo.