-
Iran: Chanzo cha uungaji mkono wowote kwa jeshi Marekani ni shabaha halali
Jul 08, 2026 14:10Makao Makuu ya Majeshi ya Iran, Khatamul-Anbiya (SAW) yametangaza kuwa chanzo chochote cha uungaji mkono unaotolewa kwa "jeshi vamizi la Marekani" katika mashambulizi dhidi ya mamlaka ya kujitawala na ardhi nzima ya Iran ni shabaha halali ya vikosi vya ulinzi.
-
Mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi: Ujumbe na Umuhimu Wake
Jul 08, 2026 11:36Misafara ya mazishi ya mwili wa Ayatollah Khamenei, Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi, imefanyika kwa kishindo katika mji mkuu Tehran na katika miji mitakatifu ya Qom nchini Iran, na Najaf na Karbala nchini Iraq, ikihudhuriwa na mamilioni ya watu wa nchi mbili hizi na vile vile wa nchi nyingine za eneo.
-
Jibu la Awali la Jeshi la Iran: Shabaha 85 za jeshi la Marekani zalengwa
Jul 08, 2026 04:49Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza rasmi kuwa, katika hatua ya kwanza ya kujibu uchokozi wa Marekani wa usiku wa kuamkia leo, vikosi vya wanamaji na anga vya Jeshi hilo, katika operesheni ya pamoja ya makombora na ndege zisizo na rubani (drones), vimetekeleza kwa mafanikio mashambulizi makali dhidi ya shabaha 85 muhimu vya kijeshi la Marekani na kutungua ndege moja ya kisasa ya kijasusi ya adui aina ya MQ9.
-
Araghchi: Wananchi na Majeshi ya Iran hawatikisiki kwa vitisho vyovyote
Jul 08, 2026 04:39Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi, amesema kuwa mamilioni ya Wairani wamekusanyika kwa umoja kutoa heshima za mwisho kwa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, na urithi wake adhimu. Akisisitiza msimamo huo, amesema kuwa wananchi wa Iran na Majeshi ya Ulinzi hawatayumbishwa na vitisho vyovyote.
-
Eslami: Maendeleo ya Nyuklia ya Iran yanatokana na mwongozo na uungaji mkono wa Kiongozi Shahidi
Jul 08, 2026 04:34Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran (AEOI) anasema kuwa sekta ya nyuklia ya Jamhuri ya Kiislamu imefikia kiwango chake cha sasa cha maendeleo kupitia mwongozo na uungaji mkono thabiti wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei.
-
Simulizi ya Kimataifa kuhusu Nguvu ya Iran: Mazishi ya Kiongozi Shahidi Yatawala Vichwa vya Habari vya Kimataifa
Jul 07, 2026 10:29Sambamba na kufanyika msafara wa mazishi ya Ali Khamenei, Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu mjini Tehran, macho ya ulimwengu mzima yalikuwa yameelekezwa Iran. Kilichofanyika mjini Tehran hayakuwa maombolezo tu bali lilikuwa tukio la kisiasa na kihistoria lililoakisiwa pakubwa kimataifa na vyombo vya habari.
-
Mamilioni wauaga mwili wa Imam Shahidi Khamenei katika mji wa Qom
Jul 07, 2026 10:00Mamilioni ya waombolezaji leo walikusanyika katika mji mtakatifu wa Qom tangu asubuhi kushiriki katika mazishi ya Kiongozi Shahidi.
-
Rais Pezeshkian kuhudhuria mazishi ya Ayatullah Khamenei nchini Iraq
Jul 07, 2026 09:43Rais Masoud Pezeshkian wa Iran alitarajiwa kusafiri kwenda Iraq leo Jumanne kuhudhuria shughuli ya mazishi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu aliyeuawa shahidi, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, iliyopangwa kufanyika katika miji mitakatifu ya Najaf na Karbala kesho Jumatano.
-
Spika wa Bunge la Iran: Wauaji wa mashahidi wa nchi hii watapata malipo ya uhalifu wao
Jul 07, 2026 09:39Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, wauaji wa mashahidi wa nchi hii watawajibishwa na watapata adhabu inayostahili kwa matendo yao.
-
Wairaqi wasubiri kwa hamu kupokea mwili wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu
Jul 07, 2026 04:34Wakati ukikaribia kwa ajili ya kufanyika mazishi ya mwili wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu katika miji ya Najaf Ashraf na Karbala Mualla, Iraq inashuhudia maandalizi makubwa yasiyokuwa ya kawaida yanayohusisha serikali, wananchi, viongozi wa makabila, vikosi vya usalama na taasisi za huduma.