-
Pezeshkian: Mataifa ya Kiislamu yanaweza kukomesha jinai za Israel
Apr 03, 2025 08:08Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian amesema umoja na mshikamano miongoni mwa mataifa ya Kiislamu unaweza kuwa chachu ya kukomeshwa jinai za kuogofya za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wananchi madhulumu wa Palestina katika Ukanda wa Gaza.
-
Iran yakosoa unafiki wa Wamagharibi kwa kufumbia macho jinai za Israel
Apr 03, 2025 03:37Iran imelaani vikali kuendelea kwa mashambulizi na jinai zinazofanywa na Israel dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan; hususan katika sikukuu za Idul-Fitri, na kutaka hatua zichukuliwe dhidi ya ukiukaji wa haki zinazofanywa na utawala huo ghasibu.
-
Kauli ya Larijani kuhusu Iran kuunda silaha za nyuklia yatikisa vyombo vya habari vya Kizayuni
Apr 02, 2025 23:58Vyombo vya habari vya Kiebrania vya utawala wa Kizayuni wa Israel vimeakisi kwa wingi kauli aliyotoa hivi karibuni Dakta Ali Larijani, Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika mahojiano na televisheni ya hapa nchini, alipotishia kwamba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itachukua hatua ya kuunda silaha za nyuklia endapo itaendelea kuandamwa na vitisho.
-
Iran: Tutatumia njia zote kuuwajibisha utawala wa Kizayuni kwa kuushambulia ubalozi wetu
Apr 02, 2025 08:29Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetoa taarifa kwa mnasaba wa kumbukumbu ya jinai iliyofanywa na utawala wa Kizayuni ya kuushambulia ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu mjini Damascus na kutangaza kuwa: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeazimia kutumia fursa na njia zote kutekeleza uadilifu na kuuwajibisha utawala wa kigaidi wa Israel.
-
Araqchi: Iran haina lengo la kumiliki silaha za nyuklia
Apr 02, 2025 03:52Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu haitaki kuunda na kumiliki silaha za nyuklia kwa hali yoyote ile.
-
Iran yaalani vikali mashambulizi ya Israel dhidi ya Lebanon
Apr 02, 2025 03:44Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani vikali mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika eneo la Dhahiya katika mji mkuu wa Lebanon, Beirut.
-
Rais wa Iran: Waislamu wanapaswa kuwa na mchango athirifu katika kukabiliana na watendajinai duniani
Apr 01, 2025 11:48Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na viongozi wa nchi mbalimbali, akiwapongeza kwa mnasaba wa kusherehekea sikukuu ya Idul-Fitr. Amesisitiza ulazima wa kuimarishwa zaidi umoja na uhusiano wa kindugu baina ya nchi za Waislamu na ulazima wa kuzima njama za maadui.
-
Araghchi: Maadui watajuta kwa kutoa vitisho dhidi ya Iran
Apr 01, 2025 08:19Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi amesisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu haitamruhusu mtu yeyote kuzungumza nayo kwa lugha ya ubabe na vitisho, akiwaonya maadui kwamba watajuta kulitishia taifa hili.
-
Wizara ya Ulinzi ya Iran: Chokochoko dhidi yetu zitakabiliwa na jibu madhubuti
Apr 01, 2025 07:23Wizara ya Ulinzi ya Iran imewaonya vikali maadui kwamba, kitendo chochote cha uchokozi dhidi ya taifa hili kitakabiliwa na jibu la haraka na madhubuti.
-
Mshauri: Ikiwa Marekani itafanya kosa, Iran itaunda silaha za Nyuklia
Apr 01, 2025 04:16Mshauri mwandamizi wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, iwapo Marekani itafanya 'kosa' lolote, Iran italazimika, kwa mashinikizo ya wananchi wake, kuelekea kwenye uundaji wa silaha za nyuklia.