-
Iran yalaani vikali vitisho vya Trump vya mashambulizi ya kijeshi
Apr 01, 2025 04:14Iran imelaani vikali vitisho vya hivi karibuni vya Rais wa Marekani, Donald Trump, vya kuishambulia nchi hii kijeshi ambapo imeviitaja kuwa ukiukaji wa wazi wa sheria za kimataifa na misingi ya Hati ya Umoja wa Mataifa.
-
National Interest: Mji wa makombora wa Iran unaonyesha nguvu ya nchi hiyo
Mar 31, 2025 23:16Gazeti la Marekani la National Interest limeuchambua mji mpya wa makombora wa Iran na kusisitiza kwamba, kufichuliwa mji huo huku hali ya wasiwasi ikiongezeka katika Bahari Nyekundu na Asia Magharibi, ni ujumbe kwa Marekani na maadui wa Iran.National Interest imekiri katika ripoti yake kwamba hifadhi ya makombora ya Iran imeongezeka kwa kiasi kikubwa katika muongo mmoja uliopita.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Iran inanyoosha mkono wa udugu kwa mataifa yote ya Kiislamu
Mar 31, 2025 08:43Mapema leo Jumatatu, katika kikao na viongozi wa serikali, mabalozi wa nchi za Kiislamu na matabaka tofauti ya wananchi wa Iran, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya kislamu, Imam Ali Khamenei amesema kuimarika heshima ya Uislamu na kukabiliana na dhulma na uonevu wa madola makubwa vinategemea umoja na utambuzi wa Umma wa Kiislamu.
-
Baqaei: Marekani ijitayarishe kwa athari za hatua yoyote dhidi ya Iran
Mar 31, 2025 08:22Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ametangaza katika ujumbe wake kwamba, tishio lolote la rais wa nchi la kuishambulia Iran kwa mabomu ni ukiukaji wa wazi na kiini cha amani na usalama wa kimataifa.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Utawala fisadi wa Israel ni ‘kikosi cha niaba tu’ katika eneo, ni lazima ung'olewe
Mar 31, 2025 03:49Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema, kikosi pekee cha niaba katika eneo hili ni utawala wa Kizayuni ambao unavamia nchi nyingine kwa niaba ya madola ya kikoloni ya dunia na ni "lazima ung'olewe."
-
Rais wa Iran atoa mkono wa Idi kwa viongozi na wananchi wa mataifa ya Kiislamu
Mar 30, 2025 23:51Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewatumia salamu za mkono wa Idi na kuwapongeza viongozi na wananchi wa mataifa ya Kiislamu kwa mnasaba wa kuadhimisha na kushereheka Idul-Fitri, siku ya sherehe na furaha kubwa kwa Waislamu.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran atoa wito wa umoja katika ujumbe wa Idul Fitr
Mar 30, 2025 23:11Katika ujumbe wa pongezi kwa wenzake Waislamu kwa mnasaba wa sikukuu ya Idul Fitr, inayoadhimisha baada ya kumalizika mwezi mtukufu wa Ramadhani, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi, ametoa wito wa kuimarisha zaidi umoja na huruma miongoni mwa mataifa ya Kiislamu.
-
Rais wa Iran: Mwelekeo wa mazungumzo unategemea mwenendo wa Wamarekani
Mar 30, 2025 23:11Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa Tehran haijawahi kukwepa mazungumzo, lakini ni aina ya mwenendo wa Wamarekani ndio unaoamua ikiwa mazungumzo yataendelea au la.
-
Majeshi ya Iran yaahidi ‘Majibu Makali’ kwa tishio lolote
Mar 30, 2025 23:11Kamandi ya Majeshi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema iko tayari kutoa jibu kali na lenye nguvu dhidi ya tishio lolote, uchokozi, au uvamizi maadui.
-
Kamanda: Iran ina uwezo wa kupiga ngome za adui popote pale
Mar 30, 2025 03:58Kamanda wa Kikosi cha Wanamaji cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) Admeli Alireza Tangsiri amesema kwa mara nyingine tena kuwa, uwezo wa kijeshi wa Iran ni wa kipekee, huku akionya dhidi ya vitisho akisisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu haiwezi kufanya mazungumzo na yeyote kuhusu maghala yake ya makombora.