-
Iran yatangaza ongezeko la watumiaji wa intaneti ya kasi ya simu za mkononi
May 18, 2025 05:45Iran imeripoti ongezeko zaidi la idadi ya watumiaji wa intaneti ya kasi ya simu za mkononi (mobile broadband) huku ikifanya juhudi za kuboresha huduma zinazotolewa na mtandao wake wa intaneti wa kasi.
-
Iran yaizamisha China kwenye mashindano ya Asia, yaingia Kombe la Dunia la Futsal kwa Wanawake 2025
May 18, 2025 01:02Timu ya taifa ya wanawake ya futsal ya Iran imemaliza katika nafasi ya tatu kwenye mashindano ya Kombe la Asia kwa Wanawake la Futsal la AFC 2025 nchini China, na hivyo kufuzu kwa mara ya kwanza kushiriki Kombe la Dunia la Wanawake la Futsal la FIFA.
-
Faida za makubaliano ya Iran na Umoja wa Kiuchumi wa Eurasia
May 17, 2025 08:30Ali Ahmadnia, Mkuu wa Masuala ya Habari wa Serikali ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametangaza kuwa takriban asilimia 87 ya bidhaa zinazouzwa kati ya Iran na nchi tano wanachama wa Umoja wa Kiuchumi wa Eurasia (EAEU) zitauzwa kati ya nchi hizo bila kutozwa ushuru.
-
Kiongozi Muadhamu: Matamshi ya Trump ni fedheha kwa taifa la Marekani
May 17, 2025 07:53Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amekosoa matamshi ya hivi karibuni ya Rais Donald Trump wa Marekani na kuyataja kuwa ni "fedheha" kwa taifa la Marekani.
-
Pezeshkian: Iran inafanya mazungumzo, lakini haigopi vitisho vyovyote
May 17, 2025 07:00Rais Masoud Pezeshkian amesisitiza kuwa, Iran haitasalimu amri na kuachana na haki zake licha ya vitisho, akieleza kuwa Jamhuri ya Kiislamu haitaachana na mafanikio yake ya heshima katika nyanja yoyote ile, iwe kisayansi au kijeshi.
-
Araqchi: Haki ya Iran ya kurutubisha urani kwa malengo ya amani si ya kufumbiwa macho
May 17, 2025 04:06Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kwamba, hakuna sinario na kitu ambacho kitaifanya Iran iachane na haki yake ya kurutubisha madini ya urani kwa malengo ya amani.
-
Spika wa Bunge Iran: Ni wajibu wa Kiislamu kusitisha ‘Mauaji Makubwa Zaidi ya Kimbari Katika Historia’
May 16, 2025 23:24Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf, ametoa wito kwa Waislamu kuimarisha umoja na kuwa sauti ya watu wa Palestina walioko Ukanda wa Gaza, ambao wanakumbwa na mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala wa Israel.
-
Azma ya Iran na nchi tatu za Ulaya kuhusu kutumia diplomasia ya nyuklia
May 16, 2025 23:20Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Kazem Gharibabadi, amesema kuwa Iran na mataifa matatu ya Ulaya ambayo Uingereza, Ufaransa, na Ujerumani (yanayojulikana kama E3), wameazimia kutumia ipasavyo njia za kidiplomasia kuhusu mpango wa nyuklia wa Tehran.
-
Abu Turabi Fard: Marekani ndiyo sababu ya ukosefu wa usalama duniani, si Iran
May 16, 2025 06:55Imam wa muda wa Sala ya Ijumaa ya hapa Tehran amesema: "Katika hali ambayo Israel inafanya mauaji ya kutisha zaidi kwa niaba ya Marekani, inazikalia kwa mabavu nchi za Kiislamu, na kukanyaga haki ya kujitawala kitaifa Lebanon, Syria na Yemen, rais wa Marekani anadai kiuongo kuwa eti Iran ndiyo tishio kwa usalama wa eneo, wakati ni Marekani ndiye tishio."
-
Iran: Israel iliundwa kwa damu; mauaji ya kimbari lazima yakomeshwe sasa
May 16, 2025 03:52Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imetoa taarifa kwa mnasaba wa Siku ya Nakba na kusema kwamba, utawala wa Kizayuni wa Israel "uliasisiwa katika msingi wa umwagaji damu" na kwamba jamii ya kimataifa ina wajibu wa kukomesha mauaji ya kimbari yanayoendelea huko Gaza.