-
Cairo, hatua ya nane ya safari ya kieneo ya Araghchi
Oct 17, 2024 23:20Seyyed Abbas Araghchi, Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewasili Cairo, mji mkuu wa Misri, katika kituo cha nane cha safari yake ya kieneo ambapo amekutana na kuzungumza na rais na waziri mwenzake wa mambo ya nje wa nchi hiyo.
-
Meja Jenerali Salami: Wazayuni wakifanya kosa, jibu letu litakuwa la kuumiza sana
Oct 17, 2024 08:14Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran (SEPAH) amesema kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel na viongozi wake wanapaswa kutambua kuwa, Operesheni ya Ahadi ya Kweli-2 lilikuwa onyo tu na kama Israel itakosea na kuthubutu kufanya uvamizi, jibu la Iran litakuwa la kuumiza sana.
-
Rais wa Iran: Moto wa vita wa Wazayuni ukomeshwe kwa kuwashinikiza wanaowaunga mkono
Oct 17, 2024 04:39Rais wa Iran ametaka kushinikizwa waungaji mkono wa utawala wa Kizayuni ili kusitisha moto wa vita na jinai za mauaji ya kimbari zinazotekelezwa na utawala huo.
-
Araqchi: Enzi za Wazungu za sera ya "kugawa na kutawala" zimekwisha
Oct 17, 2024 04:35Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa zama za siasa habithi za kugawa na kutawala za Wazungu katika eneo la Asia Magharibi zimefikia kikomo.
-
Waziri wa Ulinzi wa Iran: Mfumo wa ulinzi wa Marekani wa THAAD si jambo jipya
Oct 16, 2024 23:25Waziri wa Ulinzi wa Iran ameeleza kuwa mfumo wa ulinzi wa Marekani wa THAAD si jambo jipya na kwamba Iran unalichukulia suala hilo kuwa ni sehemu ya vita vya kisaikolojia na sio tatizo mahsusi.
-
Iran yazitaka nchi za Shanghai kuwa jadi dhidi ya jinai za Israel na ugaidi wa kiuchumi wa Marekani
Oct 16, 2024 23:24Mkuu wa ujumbe wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Mkutano wa Jumuiya ya ushirikiano ya Shanghai (SCO) huko Pakistan ameitaka jumuiya hiyo kuwa jadi na kuchukua hatua madhubuti dhidi ya chokochoko za utawala wa Kizayuni na ugaidi wa kiuchumi wa Marekani. Amezitaka nchi wanachama wa Shanghai kuchukua hatua za kivitendo ili kukabiliana na vikwazo vya kibiashara vya pande zote.
-
Iran yaonya kuhusu chokochoko mpya za Wazayuni
Oct 16, 2024 07:09Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amezungumza kwa simu na waziri mwenzake wa mambo ya nje wa Ufaransa na kuonya kuhusu matokeo mabaya na hatari mno ya chokochoko mpya za utawala wa Kizayuni katika eneo la Asia Magharibi.
-
Iran yamwita balozi wa Hungary kulalamikia vikwazo vipya vya EU
Oct 16, 2024 03:40Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imemuita balozi wa Hungary mjini Tehran na kumkabidhi malalamiko makali ya Jamhuri ya Kiislamu kwa vikwazo vipya vya Umoja wa Ulaya dhidi ya shakhsia na taasisi kadhaa za Iran.
-
Umoja wa Umma wa Kiislamu, siri ya ushindi dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel
Oct 16, 2024 00:20Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran sambamba na kuleza kuwa Iran iko tayari kusaidia kujenga maelewano ya pamoja ya kiusalama kuhusu hatari ya kihistoria ya utawala wa Kizayuni, amesema: Kuna haja kusimamishwa aina yoyote ya mpango wa kisiasa na kiuchumi unaousaidia utawala huo ghasibu.
-
Rais wa Iran ashiriki katika mazishi Shahidi Nilforoushan mjini Tehran
Oct 15, 2024 09:40Rais wa Iran amehudhuria hafla ya mazishi ya jenerali aliyeuawa shahidi Abbas Nilforoushan, mshauri wa ngazi za juu wa kijeshi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Lebanon.