-
Rais Pezeshkian: Kama Waislamu wangekuwa na umoja, Israel isingethubutu kufanya jinai yoyote
Aug 24, 2024 09:37Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: Lau Waislamu wote wangekuwa na umoja na mshikamano, basi utawala unaokalia kwa mabavu wa Israel haungethubutu kufanya jinai hizi kubwa katika ardhi za Palestina.
-
Iran yakaribisha kustawisha uhusiano na Ulaya katika anga ya kuheshimiana
Aug 24, 2024 07:51Sayyid Abbas Araqchi Waziri wa Mambo ya Nje ya serikali ya 14 ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika mazungumzo ya simu na Josep Borrell mwakilishi wa ngazi ya juu wa Umoja wa Ulaya katika masuala ya usalama na sera za je kwamba: Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inakaribisha na kuunga mkono kustaiwsha uhusiano na Umoja wa Ulaya katika mazingira ya kuheshimiana pande mbili.
-
Araghchi: Serikali mpya ya Iran ina azma ya kuimarisha uhusiano na Afrika
Aug 24, 2024 03:26Waziri mpya wa Mambo ya Nje wa Iran Abbas Araghchi amesema kuwa kipaumbele cha kwanza katika sera za kigeni ni nchi jirani na kipaumbele cha pili ni kupanua uhusiano na Afrika na Asia Mashariki. Ameongeza kuwa kipaumbele cha tatu ni nchi zilizosimama upande wa Iran katika hali ngumu.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa: Matembezi ya mamilioni ya watu ya Arubaini ya Imamu Hussein AS hayajawahi kutokea katika historia
Aug 23, 2024 10:11Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amesema, matembezi adhimu ya mamilioni ya watu ya Arubaini ya Imamu Hussein AS hayajawahi kutokea katika historia.
-
Iran yawakamata magaidi 14 wa Daesh wakipanga mashambulizi ya kigaidi
Aug 23, 2024 06:51Wizara ya Usalama wa Taifa Iran imesema imewatia mbaroni magaidi 14 wa kundi la kigaidi la Daesh au ISIS, na hivyo kuzima njama zao za kutekeleza mashambulizi ya kigaidi ndani ya nchi.
-
Iran inaunda makumi ya satelaiti kwa malengo mbali mbali
Aug 23, 2024 06:49Mkuu wa Shirika la Anga za Juu la Iran (ISA) Hossein Salariyeh anasema nchi Iran imepata maendeleo ya ajabu katika sekta ya anga katika kipindi cha miaka mitatu iliyopita na hivi sasa makumi ya satelaiti zinaendelea kuundwa nchini kwa malengo mbalimbali.
-
Kiwewe cha Wazayuni katika kusubiri jibu la kushtukiza la Iran
Aug 23, 2024 06:49Kadiri jibu la Iran kwa kitendo cha kigaidi cha utawala wa Kizayuni wa Israel linavyozidi kuchukua muda mrefu, ndivyo taathira za kimaada, kiroho na kisaikolojia zinavyozidi kuongezeka na kuwaumiza Wazayuni.
-
Eslami: Sekta ya nyuklia ya Iran iko katika kiwango cha kimataifa
Aug 23, 2024 03:05Mkuu wa Shirika la Nishati ya Atomiki la Iran amesema: Sekta ya nyuklia ya Jamhuri ya Kiislamu ni moja ya fakhari za taifa hili. Shughuli za nyuklia za Iran ni za kiwango cha kimataifa na wale waliokuwa wakibeza na kufifiliza mafanikio hayo, hivi sasa wamelazimika kubadilisha misimmamo yao na kukiri nguvu za Iran katika sekta hiyo muhimu.
-
SEPAH: Operesheni za Muqawama dhidi ya Israel zitaendelea
Aug 22, 2024 23:27Kaimu wa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH amesema kuwa, maadamu hujuma na jinai za Israel zinaendelea, operesheni za harakati za Muqawama nazo kamwe hazitosimama. Ameongeza kuwa, baada ya Operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa, majigambo ya utawala wa Kizayuni yalisambaratika kikamilifu.
-
Araqchi ataja masharti ya Iran kwa ajili ya kuhuisha uhusiano na nchi za Ulaya
Aug 22, 2024 09:39Katika mahojiano yake ya kwanza na chombo cha habari cha nje, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araqchi amesisitiza kuwa anataka kudhibiti mvutano iliyopo na Marekani na kujenga upya uhusiano na nchi za Ulaya kwa masharti.