-
SEPAH: Operesheni za Muqawama dhidi ya Israel zitaendelea
Aug 22, 2024 23:27Kaimu wa Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH amesema kuwa, maadamu hujuma na jinai za Israel zinaendelea, operesheni za harakati za Muqawama nazo kamwe hazitosimama. Ameongeza kuwa, baada ya Operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa, majigambo ya utawala wa Kizayuni yalisambaratika kikamilifu.
-
Araqchi ataja masharti ya Iran kwa ajili ya kuhuisha uhusiano na nchi za Ulaya
Aug 22, 2024 09:39Katika mahojiano yake ya kwanza na chombo cha habari cha nje, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araqchi amesisitiza kuwa anataka kudhibiti mvutano iliyopo na Marekani na kujenga upya uhusiano na nchi za Ulaya kwa masharti.
-
Kan'ani: Marekani inaunga mkono ugaidi wa kiserikali wa utawala wa Kizayuni wa Israel
Aug 21, 2024 22:50Nasser Kan'ani Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa leo hii ukweli mchungu na wa kusikitisha unashuhudiwa mbele ya walimwengu wa matabaka yote kuanzia raia wanaoteseka na kudhulumiwa katika eneo la Magharibi mwa Asia, kaskazini mwa Afrika hadi kwa wanafunzi wa vyuo vikuu barani Ulaya na Marekani kwamba serikali ya Marekani inaunga mkono waziwazi ugaidi wa kiserikali wa utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Umoja wa Mataifa wapongeza ukarimu wa Iran kwa wakimbizi
Aug 21, 2024 22:48Afisa msimamizi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR hapa nchini Iran ameipongeza Jamhuri ya Kiislamu kwa kuwapokea kwa ukarimu na kuwa mwenyeji wa wakimbizi.
-
Mawaziri wa Rais Pezeshkian waidhinishwa na bunge la Iran
Aug 21, 2024 09:59Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) imehitimisha mjadala kuhusu baraza jipya la mawaziri la serikali ya awamu ya 14 kwa kuidhinisha mawaziri 19 waliopendekezwa na Rais Masoud Pezeshkian.
-
Mazuwari 28 raia wa Pakistan waaga dunia katika ajali ya basi Iran
Aug 21, 2024 08:23Raia 28 wa Pakistan wamepoteza maisha huku makumi ya wengine wakijeruhiwa baada ya basi lililokuwa limewabeba kubingiria katika kaunti ya Taft, mkoani Yazd, katikati ya Iran. Mazuwari hao walikuwa wakielekea katika mji mtakatifu wa Karbala nchini Iraq kwa ajili ya kushiriki Arubaini ya Imam Hussein AS.
-
Iran: Mbinu na muda wa jibu letu vitaishangaza mno Israel
Aug 21, 2024 04:23Ofisi ya Uwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa imesema Jamhuri ya Kiislamu inapanga kwa makini muda na mbinu ya kulipiza kisasi cha mauaji ya kigaidi ya aliyekuwa Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Wapalestina (HAMAS), Ismail Haniyah akiwa hapa Tehran.
-
Iran yakanusha madai ya kufanya udukuzi katika kampeni za uchaguzi wa rais Marekani
Aug 20, 2024 08:52Ofisi ya Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa imepinga vikali madai kwamba Jamhuri ya Kiislamu inaingilia uchaguzi wa rais wa Marekani wa 2024, na kuyataja madai hayo kuwa "hayana msingi."
-
Iran, Malaysia zalaani msaada wa kijeshi wa madola ya Magharibi kwa Israel
Aug 20, 2024 03:41Iran na Malaysia zinakubaliana kwamba msaada wa silaha unaotolewa na Marekani na nchi nyingine za Magharibi kwa utawala wa Kizayuni Israel unakinzana na madai yao kuhusu haki za binadamu na pia msaada huo unadhoofisha juhudi za usitishaji vita huko Gaza.
-
IRGC: Israel isubiri jibu kali kwa kumuua kiongozi wa Hamas
Aug 20, 2024 03:38Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limesisitiza kuwa litalipiza kisasi mauaji yaliyotekelezwa na utawala wa Israel dhidi ya kiongozi wa ngazi ya juu wa Hamas, Ismail Haniyeh katika mji mkuu wa Iran, Tehran kwa jibu litakalokuwa kali na la nguvu zaidi kuliko wakati uliopita ambapo Jamhuri ya Kiislamu ililipiza kisasi dhidi ya uchokozi wa Tel Aviv.