-
Kamanda Mkuu wa Jeshi la Iran aahidi uungaji mkono endelevu kwa Muqawama
Nov 25, 2024 07:48Israel imefikia katika hali ya mkwamo, na Jamhuri ya Kiislamu itaendelea daima kuunga mkono mapambano halali na ya haki dhidi ya utawala wa kibaguzi wa Israel.
-
Iran yakanusha madai ya kuhusika katika mauaji ya kuhani wa Israel huko Abu Dhabi
Nov 25, 2024 04:37Ubalozi wa Iran mjini Abu Dhabi katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) umepinga madai ya kuhusika kwa namna yoyote na mauaji ya kuhani wa Kizayuni mjini Abu Dhabi.
-
Iran: Dunia isimame kutetea wanawake wa Kipalestina
Nov 25, 2024 04:36Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran ametuma ujumbe katika mtandao wa kijamii wa X kwa mnasaba wa Siku ya Kimataifa ya Kupigwa Marufuku Ukatili dhidi ya Wanawake ambayo huadhimishwa kila mwaka tarehe 25 Novemba, akizungumzia jinai zinazofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya wanawake na wasichana wa Palestina hasa katika Ukanda wa Gaza.
-
Araghchi kushiriki mkutano wa UNAOC nchini Ureno
Nov 25, 2024 00:21Abbas Araghchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran anatazamia kuelekea nchini Ureno kushiriki katika mkutano wa 10 wa kimataifa wa Kongamano la Muungano wa Umoja wa Mataifa wa Ustaarabu (UNAOC).
-
Venezuela yapongeza misimamo ya Iran kuhusu uingiliaji wa Washington katika masuala ya ndani ya Caracas
Nov 25, 2024 00:03Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Venezuela amepongeza misimamo ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kukabiliana na uingiliaji kati wa serikali ya Marekani katika masuala ya ndani ya Venezuela.
-
Russia yakosoa hatua ya Magharibi dhidi ya Iran katika Bodi ya Magavana ya IAEA
Nov 25, 2024 00:03Ubalozi wa Russia mjini Tehran umekosoa hatua ya nchi za Magharibi dhidi ya Iran katika Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Nyuklia (IAEA).
-
Utekelezaji wa hukumu ya Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC), mtihani kwa Wamagharibi
Nov 24, 2024 10:24Ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya haki za binadamu huko Palestina amesema kuwa utekelezaji na kushikamana nchi za Magharibi na uamuzi wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) wa kuwakamata viongozi wa utawala wa Kizayuni ni mtihani wa kupima azma na uwajibikaji wa Wamagharibi kuhusu hukumu hiyo.
-
Brigedia Jenerali Reza Sadeghi: US imetumia dola trilioni tisa Asia Magharibi bila mafanikio yoyote
Nov 24, 2024 07:05Mshauri mwandamizii wa Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) amesema: Wamarekani hawajapata mafanikio licha ya kutumia dola trilioni tisa katika eneo la Magharibi mwa Asia.
-
Spika Qalibaf: Uwekaji wa mashinepewa za kisasa ni jibu kwa ufanyaji mambo kisiasa wa IAEA
Nov 24, 2024 06:35Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran amesema, kuanza kutumiwa mashinepewa (centrifuges) mpya na za kisasa ni jibu la Jamhuri ya Kiislamu kwa hatua ya baadhi ya nchi ya kuitumia kisiasa Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA).
-
Iran: Tunakaribisha hatua zozote za kuondolewa kinga utawala wa Kizayuni
Nov 24, 2024 03:57Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu inakaribisha hatua yoyote ya kuuondolea kinga utawala wa Kizayuni na kuiwajibisha Israel kwa jinai zake za kivita na mauaji ya kizazi huko Palestina.