-
Kinu cha nyuklia cha Iran chavunja rekodi ya kuzalisha umeme
Aug 16, 2024 00:42Kinu cha nyuklia cha Bushehr cha kusini mwa Iran kimevunja rekodi ya kuzalisha umeme kati ya vinu vyote vya nishati hiyo humu nchini ambapo katika kipindi cha siku 60 zilizopita kimeweza kuzalisha megawati 1,395,290 umeme ambao unatosheleza matumizi ya familia milioni 203.
-
Bagheri Kani: Kunyamazia ukatili wa Wazayuni kunaipa kiburi zaidi Israel
Aug 15, 2024 10:46Kaimu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema kuwa, uzoefu unaonyesha kuwa, kimya dhidi ya ukatili wa kijeshi na kiusalama wa Wazayuni kunaufanya utawala huo muovu kuwa na jeuri zaidi.
-
Kan’ani: Utawala wa Kizayuni unafanya jinai dhidi ya binadamu kwa uungaji mkono wa Marekani
Aug 15, 2024 09:55Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema: Utawala wa kigaidi na kibaguzi wa Israel unajishughulisha na kutenda jinai dhidi ya binadamu kwa uungaji mkono kamili wa serikali ya Marekani.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu alihimiza taifa la Iran kusimama kidete katika vita vya kisaikolojia vya adui
Aug 15, 2024 06:35Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Ali Khamenei, amezungumzia hila na njama za wasiolitakia mema taifa la Iran katika kuanzisha vita vya kisaikolojia na kutaka kulirudisha nyuma katika nyuga mbalimbali na kusema, utambuzi wa uwezo wa ndani na kuepuka kutia chumvi nguvu za maadui ndiyo njia pekee ya kukabiliana na njama hizo.
-
Jenerali Ghorbani: Vikwazo vimeimarisha mfumo wa kijeshi wa Iran
Aug 15, 2024 04:15Naibu Mratibu wa Kikosi cha Nchi Kavu cha Jeshi la Iran amesema kuwa vikwazo vya kikatili dhidi ya Iran havijakuwa na matokeo mengine ghairi ya kuimarisha mifumo ya kijeshi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Baadhi ya Wairani kwenda Arubaini, Iraq kwa njia ya bahari
Aug 15, 2024 04:13Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imefungua njia ya baharini kutoka Bandari ya Khorramshahr, Magharibi mwa Iran hadi Bandari ya Basra nchini Iraq kwa ajili ya safari ya majini ya Mazuwari wa Kiirani wanaoenda kushiriki Arubaini ya Imam Hussein AS.
-
Iran yatuma barua za malalamiko kwa maafisa wa haki za binadamu wa UN
Aug 14, 2024 11:27Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa mjini Geneva Uswisi amewatumia barua kwa nyakati tofauti maafisa wa haki za binadamu akibainisha malalamiko makubwa ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa hatua na sera zisizo z akibinadamu za utawala wa Kizayuni na hasa mauaji ya kigaidi ya Ismail Haniyeh kiongozi wa kisiasa wa Hamas.
-
Iran imetoa mikopo ya dola bilioni 28.7 kwa biashara, viwanda na familia katika kipindi cha miezi minne
Aug 14, 2024 11:26Takwimu za Benki Kuu ya Iran zinaonyesha kuwa kaya nchini zilipata asilimia 22.7 ya jumla ya mikopo iliyotolewa na mfumo wa benki nchini katika kipindi cha miezi minne hadi Julai 21.
-
Kiongozi Muadhamu atilia mkazo wajibu wa kusimama imara mbele ya vita vya kisaikolojia vya adui
Aug 14, 2024 09:00Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametilia mkazo wajibu wa kusimama imara kukabiliana na vita vya kisaikolojia vya adui akisema kuwa, wanaoendesha vita hivyo dhidi ya Iran wanajaribu kuzusha hofu na kulifanya taifa hili lilegeze kamba na lirudi nyuma katika nyuga tofauti.
-
Bagheri Kani: Uvamizi wa Wazayuni katika Msikiti wa Al-Aqsa unalenga kuzidisha mivutano
Aug 14, 2024 04:07Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema uvamizi wa baadhi ya mawaziri wa serikali ya utawala bandia wa Israel na walowezi wa Kizayuni katika msikiti wa al Aqsa ni hatua ya kichochezi inayolenga kushadidisha mivutano na ukosefu wa amani katika eneo.