-
Araqchi akanusha Iran kuipatia Russia makombora ya balistiki
Oct 13, 2024 09:28Iran kwa mara nyingine tena imekadhibisha madai kuhusu kuipatia Russia makombora ya balistiki kufuatia ripoti kwamba Umoja wa Ulaya utatumia tuhuma hizo kama kisingizio cha kuwekea vikwazo Jamhuri ya Kiislamu.
-
Mkakati wa Iran ni kuunga mkono muqawama na kukabiliana na hatua za utawala wa Kizayuni za kuibua mivutano katika eneo
Oct 13, 2024 08:02Mkakati wa siku zote wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni kuunga mkono muqawama kwa lengo la kukabiliana na siasa za utawala wa Kizayuni za kuibua vita na migogoro katika eneo.
-
Iran yakanusha madai ya kuhusika na operesheni ya Wapalestina ya Kimbunga cha Al Aqsa
Oct 13, 2024 03:40Ujumbe wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa umepuuzilia mbali ripoti za vyombo vya habari vya Marekani zinazodai kuwa Jamhuri ya Kiislamu ilikuwa na taarifa kuhusu Operesheni ya Kimbunga cha al-Aqsa iliyotekelezwa mwaka jana na wapigania ukombozi wa Palestina dhidi ya utawala wa Israel.
-
Iran: Tutatoa jibu madhubuti kwa nchi zitakazokubali kutumiwa kutushambulia
Oct 12, 2024 23:14Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema Jamhuri ya Kiislamu itajibu mapigo dhidi ya nchi ambazo zitaruhusu anga na ardhi zao zitumiwe kulishambulia taifa hili.
-
Iran kujenga hospitali nyingine nchini Lebanon baada ya Israel kushambulia hospitali ya IRCS
Oct 12, 2024 22:45Mkuu wa Shirika la Hilali Nyekundu la Iran (IRCS) ametangaza mipango ya kuanzisha hospitali mpya ya kuwahudumia Walebanoni walioathiriwa na vita yya kikatili vya Israel.
-
Rais wa Iran: Vyuo vikuu vinapasa kuifikisha nchi katika kilele cha sayansi na teknolojia
Oct 12, 2024 09:31Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa chuo kikuu kinapasa kuiweka nchi katika kilele sayansi na teknolojia.
-
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) awasili mjini Beirut, Lebanon
Oct 12, 2024 08:18Mohammad Bagher Ghalibaf Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) ambaye yupo njiani kuelekea Geneva kushiriki Mkutano wa Kilele wa Mabunge ya Dunia, amewasili mjini Beirut kabla ya kuelekea Uswisi kwa ajili ya kuonana na kuzungumza na viongozi wa Lebanon na kutangaza uungaji mkono wake kwa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon.
-
Iran: Walimwengu wachukue hatua kukabiliana na jinai za utawala wa Kizayuni
Oct 12, 2024 03:52Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema kuwa, walimwengu wanapaswa kuchukua hatua za pamoja kukabiliana na hatua za kishari na jinai za utawala haramu wa Israel.
-
Pezeshkian, Putin wapongeza uhusiano wa ‘kimkakati’ kati ya Iran na Russia
Oct 11, 2024 23:23Rais Vladmir Putin wa Russia amemwambia Rais mwenzake wa Iran, Masoud Pezeshkian kwamba uhusiano na Iran ni kipaumbele kwa Russia na uhusiano huu sasa unaendelea kwa mafanikio.
-
Rais wa Iran asisitizia umuhimu wa umoja wa Waislamu
Oct 11, 2024 07:48Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian amesisitiza haja ya umma wa Kiislamu kuwa na umoja na mshikamano na kubainisha kwamba, migawanyiko kati ya Waislamu itawanufaisha maadui pekee.