-
Zaidi ya wageni 300 kushiriki hafla ya kuapishwa Rais mpya wa Iran
Jul 27, 2024 23:46Zaidi ya wageni 300 watahudhuria hafla ya kuapishwa rais mteule wa Iran Dakta Masoud Pezeshkian.
-
Tehran: Tuhuma za utawala wa Israel unaouawa watoto dhidi ya Iran ni kichekesho
Jul 27, 2024 03:46Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema kuwa, tuhuma zilizotolewa na waziri wa utawala wa Israel unaoua watoto dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuhusiana na Michezo ya Olimpiki ya Paris 2024 ni jaribio lililofeli la kupotosha fikra za umma za walimwengu kuhusiana na mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala huu huko Gaza.
-
Iran yapongeza makubaliano ya makundi ya Palestina ya Beijing China
Jul 26, 2024 23:06Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amekitaja kikao cha hivi karibuni cha makundi ya Palestina mjini Beijing China na makubaliano yaliyofikiwa kuwa ni katika mwelekeo wa mapatano na maridhiano ya kitaifa. Nasser Kan'ani Chafi amesema hiyo ni hatua yenye thamani kubwa na "harakati ya kuelekea katika mwelekeo sahihi".
-
Sisitizo la Iran la ulazima wa "kupigwa buti" sarafu ya dola katika mabadilishano ya biashara
Jul 26, 2024 22:53Naibu Gavana wa Benki Kuu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa kuna udharura kwa nchi za dunia kufanya biashara na kuendesha miamala baina yao kwa kutegemea sarafu za nchi zao na si kwa kutumia dola ya Marekani au Euro ya Ulaya.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa Tehran: Rais mteule wa Iran ametokana na kura za wananchi
Jul 26, 2024 09:27Khatibu wa Sala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amesema, rais mteule wa Iran amechaguliwa kwa kura za wananchi.
-
Iran yalaani hatua ya Ujerumani kufunga Kituo cha Kiislamu Hambrug
Jul 26, 2024 04:17Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Ali Bagheri Kani amelaani vikali hatua ya polisi ya Ujerumani ya kupiga marufuku Kituo cha Kiislamu cha Hamburg (IZH) na asasi zake tanzu, na kusema kwamba hatua hiyo inakiuka kanuni za kimsingi za uhuru wa kuabudu.
-
Iran yakanusha madai ya njama ya kuwalenga wanariadha wa Israel katika michezo ya Olimpiki
Jul 26, 2024 04:16Iran imekanusha vikali madai ya njama ya kuwalenga wanariadha na watalii wa utawala wa Kizayuni wa Israel wakati wa Michezo ya Olimpiki ya Paris.
-
Pezeshkian awahutubu wabunge wa US: Damu ya wasio na hatia haitaacha katu kumwandama dhalimu
Jul 26, 2024 09:31Rais Mteule wa Iran Masoud Pezeshkian ametoa mjibizo kwa kitendo cha wabunge wa Marekani cha kumshangilia waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni alipohutubia bunge la nchi hiyo na kusisitiza kwamba: "damu ya wasio na hatia haitaacha katu kumwandama dhalimu."
-
Kiongozi Muadhamu: Uungaji mkono wa ulimwengu kwa Palestina unatokana na moyo wa Mapinduzi ya Kiislamu
Jul 26, 2024 00:54Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema harakati zinazofanywa duniani siku hizi kwa manufaa ya Palestina ni matokeo ya moyo wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Iran yalaani hotuba ya Netanyahu katika Kongresi ya Marekani
Jul 25, 2024 07:50Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema: Benjamin Netanyahu, mtenda jinai nambari moja wa utawala bandia wa Israel, amepakatwa kwenye mikono ya waungaji mkono wake baada ya miezi 9 ya mauaji ya kimbari na mauaji ya watoto wachanga; na fedheha ndilo neno dogo linaloweza kutumiwa kueleza kashfa hiyo.