-
Viongozi wa nchi 68 watoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Sayyid Raisi na ya wenzake
May 22, 2024 11:26Viongozi na maafisa wakuu wa nchi 68 duniani leo wamefika kwenye ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Tehran kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Rais Sayyid Ebrahim Raisi na ya wenzake waliokufa shahidi pamoja naye katika ajali ya helikopta iliyotokea siku ya Jumapili.
-
Kiongozi wa Mapinduzi amhutubu Haniya: Ahadi ya Allah ya kutokomezwa utawala wa Kizayuni itatimia
May 22, 2024 09:16Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza katika mazungumzo na Ismail Haniya, Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Hamas na ujumbe alioandamana nao kwamba ahadi ya Mwenyezi Mungu ya kutokomezwa utawala wa Kizayuni itatimia.
-
Ujumbe wa rambirambi wa serikali na taifa la Iraq kwa Kiongozi Muadhamu na taifa la Iran
May 22, 2024 07:11Kufuatia kufa shahidi Rais Ebrahim Raisi wa Iran na wenzake katika ajali ya helikopta, Waziri Mkuu wa Iraq, Mohammad Shia al-Sudani, amefika Tehran na kukutana na Ayatullah Khamenei Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, na kumpa salamu za rambirambi kwa niaba ya serikali na taifa la Iraq.
-
Kikao cha kwanza cha Baraza la Mawaziri Iran chaongozwa na kaimu Rais Mohammad Mokhber
May 22, 2024 07:06Kikao cha kwanza cha baraza la mawaziri la serikali ya Iran baada ya kufa shahidi Sayyid Ebrahim Raisi kimefanyika chini ya uenyekiti wa kaimu rais Mohammad Mokhbar na kuwashirikisha wanabaraza wote.
-
Ismail Haniyah: Raisi Raisi aliamini Palestina kuwa suala kuu la Kiislamu ulimwenguni
May 22, 2024 06:53Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas , Ismail Haniyah amepongeza misimamo ya marehemu rais wa Iran Shahidi Ebrahim Raisi ya kuunga mkono Palestina.
-
Uwezo wa kisheria wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wa kikabiliana na matukio yasiyotabirika
May 22, 2024 05:00Kuanza kazi kwa awamu ya 6 ya Baraza la Wataalamu Wanaomchagua Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu na kuainishwa tarehe 28 June kuwa tarehe ya kufanyika uchaguzi mpya wa Rais nchini kunaonyesha wazi uwezo mkubwa wa kisheria wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kukabiliana na matukio yanayojitokeza katika nyakati tofauti.
-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu aongoza swala ya maiti ya mashahidi wa ajali ya helikopta
May 22, 2024 04:23Ayatullah Khamenei Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu leo asubuhi ameongoza swala ya maiti na kuwaombea maghfira kwa Mwenyezi Mungu mashahidi Rais Sayyid Ebrahim Raisi na wenzake.
-
Wakazi wa mji mkuu wa Iran watoa heshima za mwisho kwa Ebrahim Raisi na wenzake
May 22, 2024 03:53Wananchi na wakazi wa mji wa Tehran leo wametoa heshima za mwisho na kuaga mwili wa Ebrahim Rais pamoja na wenzake walioaga dunia katika ajali ya helikopta siku ya Jumapili.
-
Waislamu wa Tanzania wamuomboleza Sayyid Ebrahim Raisi
May 22, 2024 03:39Waislamu nchini Tanzania wameshiriki katika hafla ya kuwakumbuka na kuwaenzi viongozii wa Iran walioaga dunia hivi karibuni akiwemo Rais Ebrahim Raisi.
-
Wairani wawaomboleza na kuwaaga shahidi Raisi na wenzake katika mji wa Tabriz
May 21, 2024 09:10Mamilioni ya wananchi wa Iran wameshiriki katika msafara mkubwa wa kuawaaga na kutoa heshima za mwisho kwa shahidi Ebrahim Raeisi na wenzake ambao walikufa shahidi katika ajali ya helikopta katika eneo milimani katika mkoa wa Azarbaijan Mashariki, kaskazini-magharibi mwa Iran.