-
Raisi: Wote ni washindi katika uchaguzi wa Iran kwani wametekeleza wajibu
Mar 01, 2024 06:41Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa uchaguzi katika Jamhuri ya Kiislamu hauna walioshindwa na kwamba hakuna tofauti yoyote kuhusu nani atashinda.
-
Kan'ani: Jeraha la Gazah halitafutika katika kumbukumbu za watu huru
Mar 01, 2024 03:48Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema kuwa, jeraha la Gazah halitafutika katika kumbukumbu za watu huru.
-
Kiongozi Muadhamu: Macho ya walimwengu yanaitazama Iran
Mar 01, 2024 03:15Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amepiga kura yake katika dakika za awali za upigaji kura kwa ajili ya awamu ya 12 ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge) na awamu ya 6 ya Baraza la Wataalamu wa Uongozi.
-
Uchaguzi nchini Iran unafanyika leo Ijumaa
Mar 01, 2024 00:17Uchaguzi wa duru ya 12 ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge) na Baraza la Wataalamu Wanaomchagua Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu unafanyika leo Ijumaa kote nchini ambapo wagombea watawania viti 290 vya Bunge na 88 vya Baraza la Wataalamu Wanaomchagua Kiongozi Mkuu wa nchi.
-
Iran yatuma angani salalaiti ya utafiti ya Pars-1 iliyotengenezwa nchini
Feb 29, 2024 23:31Iran jana Alhamisi ilifanikiwa kurusha angani salalaiti yake ya utafiti iliyotengenezwa na wataalamu wa hapa nchini.
-
Kuchaguliwa wagombea wanaofaa, mdhamini wa maslahi ya taifa
Feb 29, 2024 22:58Sambamba na kufanyika leo tarehe Mosi Machi uchaguzi wa awamu ya kumi na mbili ya Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu na awamu ya sita ya Baraza la Wataalamu Wanaomchagua Kiongozi Muadhamu, suala la kuchagua wagombea wanaofaa ni moja ya nukta muhimu ambazo zimekuwa zikitiliwa mkazo na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika uchaguzi huu na chaguzi nyingine zote zilizopita.
-
Kampeni za uchaguzi wa Bunge Iran zimemalizika, kesho kinyang'anyiro
Feb 29, 2024 08:39Kampeni za uchaguzii wa Bunge na Baraza la Wataalamu Wanaomchagua Kiongozi Mkuu wa Iran zimemalizika mapema leo saa mbili asubuhi, masaa 24 kabla ya kung'oa nanga ya kinyang'anyiro hicho.
-
Ukosoaji wa Iran kwa Baraza la Usalama la UN kwa kutochukua hatua kuhusiana na mauaji ya kimbari ya Wapalestina wa Ghazza
Feb 29, 2024 03:44Tangu ilipoanza duru mpya ya mauaji ya kimbari ya Wapalestina yanayofanywa na wanajeshi wa utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Ghazza, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imekuwa ikitumia kila fursa inayopata kulaani jinai za utawala huo ghasibu na kutaka mashambulizi ya kinyama yanayofanywa dhidi ya Wapalestina yakomeshwe.
-
Marekani yatumia $12m kuwalinda wahalifu waliohusika na mauaji ya Jenerali Soleimani
Feb 29, 2024 03:43Ripoti zinasema Idara ya Huduna za Siri ya Marekani inaripotiwa kutumia zaidi ya dola milioni 12 ili kuwalinda washauri wawili wa usalama wa rais wa zamani wa nchi hiyo, Donald Trump kwa kuhofia "vitisho" dhidi ya maisha yao kutoka Iran kwa ajili ya kulipiza kisasi mauaji ya kamanda mkuu wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Luteni Jenerali Qassem Soleimani aliyeuawa kigaidi na ndege isiyo na rubani ya Marekani akiwa safarini nchini Iraq.
-
Safari za ndege baina ya Iran na Oman zaongezeka maradufu, biashara yazidi kustawi
Feb 28, 2024 23:33Wakuu wa mashirika ya ndege ya Iran na Oman wamesema kuwa, safari za ndege baina ya nchi hizi mbili ndugu za Kisilamu zimeongezeka maradufu hivi sasa kutoka safari 30 hadi 60 kwa wiki.