-
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu: Maadui wa Iran wanaogopa ushiriki wa watu katika uchaguzi
Feb 28, 2024 10:16Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesema: Maadui wa Iran ya Kiislamu wana hofu ya kushiriki kwa wingi kwa wananchi katika uchaguzi hapa nchini.
-
Kanani ajibu matamshi ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani dhidi ya Iran
Feb 28, 2024 08:26Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Nasser Kanani ametaja tuhuma za Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kikao cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kuwa ni jaribio lisilozaa matunda la kuficha uungaji mkono wa nchi hiyo kwa utawala wa Kizayuni na kutojali ukiukaji mkubwa wa haki za binadamu huko Palestina.
-
Usalama kwenye uchaguzi; mafanikio muhimu ya kisiasa ya Iran
Feb 28, 2024 06:37Moja ya mafanikio na matunda muhimu zaidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika kipindi cha miaka 45 iliyopita ni kufanyika chaguzi 39 katika mazingira salama na ya amani kamili.
-
"Kamishna wa Haki wa UN achukue hatua za kukomesha jinai za Israel Gaza"
Feb 28, 2024 03:45Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amemtaka Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa achukue hatua madhubuti za kukomesha jinai za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.
-
Amir-Abdollahian: Uhusiano bora wa Iran na Misri utaathiri vyema eneo zima
Feb 27, 2024 23:23Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Hossein Amir-Abdollahian amesema uhusiano wa kidiplomasia kati ya Jamhuri ya Kiislamu na Misri utaathiri vyema eneo zima.
-
Kukua uchumi wa Iran licha ya kuandamwa na vikwazo
Feb 27, 2024 23:19Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) limetangaza kuwa, uchumi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran umekuwa kwa kiwango ambacho haikutabiriwa
-
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran: Dhamiri zilizoamka zinapinga mauaji ya kimbari ya Wapalestina
Feb 27, 2024 09:12Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nchi za Nje ya Iran amekitaja kilio cha rubani wa Marekani aliyejitoa mhanga kwa kujichoma moto mbele ya ubalozi wa Israel mjini Washington akipinga mauaji ya kimbari yanayofanywa na utawala huo dhidi ya watu wa Palestina huko Gaza kuwa ni sauti kubwa ya dhamiri zilizoamka nchini Marekani zinazopinga uungaji mkono wa serikali nchi hiyo kwa mauaji ya kimbari ya Wapalestina.
-
Kwesi Pratt: Iran ina mfumo madhubuti wa demokrasia
Feb 27, 2024 07:50Mwandishi mashuhuri wa habari wa Ghana amesema, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina mfumo madhubuti wa demokrasia.
-
Kubainishwa misimamo ya Iran kuhusu haki za binadamu katika Mkutano wa Geneva
Feb 27, 2024 05:36Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amewasilisha misimamo na mitazamo ya Iran kuhusu haki za binadamu katika mkutano wa 55 wa Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa mjini Geneva Uswisi.
-
Iran yaionya UN: Marekani inashadidisha taharuki katika eneo
Feb 27, 2024 03:59Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amekosoa vikali juhudi za Marekani za kushadidisha hali ya taharuki katika Bahari Nyekundu na Yemen na kuonya kuwa, hatua hizo za kijeshi za Washington hazitakuwa na matokeo mengine isipokuwa kuvuruga jitihada za pamoja za Iran na Umoja wa Mataifa katika eneo la Asia Magharibi.