-
Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran yalaani vikali mashambulizi ya kijeshi ya Marekani dhidi ya Venezuela
Jan 03, 2026 08:12Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa taarifa ikilaani vikali mashambulizi ya kijeshi ya Marekani dhidi ya Venezuela na ukiukaji mkubwa wa mamlaka ya kujitawala na umoja wa ardhi nzima ya nchi hiyo.
-
Iran yaihutubu UN kuhusu 'mwenendo haramu endelevu' wa Trump
Jan 03, 2026 03:31Iran imeuonya rasmi Umoja wa Mataifa kuhusu "mwenendo haramu endelevu" wa Marekani, kufuatia matamshi ya vitisho ya Rais Donald Trump ambayo Jamhuri ya Kiislamu imeyashutumu na kuyaeleza kama ya uingiliaji wa mambo yake ya ndani na tishio la wazi la utumiaji nguvu.
-
Iran, ulimwengu wa Kiislamu waadhimisha kumbukizi ya kuzaliwa Imam Ali AS
Jan 03, 2026 02:34Wananchi Waislamu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wamejiunga na wenzao kote duniani kuadhimisha siku ya kukumbuka kuzaliwa Amirul Muumin Ali (AS) Imam wa Kwanza wa Waislamu wa Kishia ulimwenguni.
-
Araghchi amjibu Trump: Vikosi vya Iran viko tayari kujibu mapigo
Jan 02, 2026 23:24Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi amemuonya Rais wa Marekani, Donald Trump dhidi ya kuingilia masuala ya ndani ya Jamhuri ya Kiislamu, akikosoa matamshi yake ya hivi karibuni na kuyaeleza kuwa "yasiyo na busara na hatarishi," na kusisitiza kwamba vikosi vya jeshi la Iran vimejiandaa kikamilifu kulinda mamlaka ya kujitawala nchi hii.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa: Adui anatamani kuyageuza matatizo ya kiuchumi kuwa mgogoro wa kiusalama
Jan 02, 2026 09:25Khatibu wa Sala ya Ijumaa mjini Tehran amesema maadui wa Iran wanajaribu kutumia matatizo ya kiuchumi ili kuibua mzozo wa kiusalama nchini
-
Onyo kuhusu matokeo mabaya ya vitisho vya Marekani dhidi ya mpango wa nyuklia wa amani wa Iran
Jan 02, 2026 08:59Tehran imeonya kuhusu matokeo mabaya ya vitisho vya hivi karibuni vya Marekani dhidi ya mpango wa nyuklia wa amani wa Iran.
-
Wairani wamkumbuka na kumuenzi Haj Qassem Soleimani
Jan 02, 2026 07:29Maelfu ya watu kutoka Iran na kote ulimwenguni wamekusanyika katika mji wa Kerman ulioko kusini mwa Iran, kuadhimisha kumbukizi ya kuuawa shahidi Luteni Jenerali Qassem, aliyekuwa kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC.
-
Iran yajibu bwabwaja, vitisho na matamshi ya uingiliaji ya Trump
Jan 02, 2026 06:47Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran ameonya kwamba, uingiliaji kati wa Marekani katika masuala ya ndani ya Jamhuri ya Kiislamu utavuruga utulivu wa eneo zima la Asia Magharibi na kuhatarisha moja kwa moja maslahi ya Marekani katika eneo.
-
Jenerali Vahidi: Vitisho vya Maadui vinatokana na woga na hofu yao
Jan 02, 2026 03:24Naibu kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH, amesisitizia wajibu wa kuendelea Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuunga mkono Mhimili wa Muqawama na kusema kuwa: "Vitisho na bwabwaja za maadui zinatolewa kutokana na woga na hofu waliyo nayo na hazitaathiri njia ya Jamhuri ya Kiislamu na ya Kambi ya Muqawama."
-
Pezeshkian: Jenerali Soleimani alikuwa nembo ya maelewano na utiifu kwa Kiongozi Muadhamu
Jan 01, 2026 23:18Rais Masoud Pezeshkian amesisitiza kwamba, taifa la Iran litaendeleza njia ya Shahid Luteni Jenerali Qassem Soleimani aliyekuwa kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu SEPAH na viongozi wengine wa kambi ya Muqawama akiongeza kuwa, shahidi Soleimani alikuwa nembo ya maelewano, huruma na utiifu kwa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu.