-
IRGC: Maadui watakabiliwa na mwelekeo mpya wa uwezo wa Iran iwapo wataanzisha vita
Dec 15, 2025 07:30Msemaji wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu IRGC Ali-Mohammad Naeini amesema kwamba ikiwa vita vitazuka, adui atakabiliwa na viwango vipya na vya hali ya juu vya nguvu ya kijeshi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Velayati: Iran inaiunga mkono Hizbullah ya Lebanon kwa dhati
Dec 15, 2025 03:26Mshauri wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu katika Masuala ya Kimataifa amesema kuwa, Hizbullah ni moja ya nguzo muhimu zaidi za kambi ya Muqawama na ina jukumu la kimsingi katika kukabiliana na Uzayuni. Hivyo Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, chini ya maagizo ya Kiongozi Muadhamu, itaendelea kuiunga mkono harakati hiyo ambayo iko mstari wa mbele katika Muqawama.
-
Kiwanda kikubwa cha nishati ya jua cha Iran kuzalisha umeme wa nyumba milioni 2.5
Dec 15, 2025 03:20Iran iko mbioni kukamilisha ujenzi wa kiwanda kikubwa cha nishati ya jua katika mkoa wa Isfahan wa katikati mwa Iran, mradi ambao unaotarajiwa kuzalisha umeme kwa karibu nyumba milioni 2.5 humu nchini.
-
Aragchi: Ushirikishwaji wa Afghanistan ni msingi wa uthabiti wa kudumu
Dec 14, 2025 22:55Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araqchi, amesema uthabiti wa Afghanistan unategemea kuingizwa kwake kikamilifu katika mifumo ya kisiasa na kiuchumi ya kikanda, akisisitiza umuhimu wa ushirikiano wa majirani badala ya kutegemea nguvu za nje.
-
Iran yalaani shambulio la “kikatili” dhidi ya hafla ya Kiyahudi nchini Australia
Dec 14, 2025 22:47Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imelaani shambulio la “kikatili” lililolenga hafla ya Kiyahudi mjini Sydney, Australia, shambulio ambalo limeua watu wasiopungua 12 na kuwajeruhi wengine kadhaa.
-
Ushirikiano kati ya Iran na wanachama wa BRICS: Mkakati wa kuimarisha ushirikiano wa pande nyingi
Dec 14, 2025 08:38Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza katika mazungumzo yake na Spika wa Baraza la Wawakilishi la Ethiopia kwamba: BRICS inaweza kuandaa mazingira ya kuwepo ushirikiano wa haki na wenye uwiano katika ngazi ya kimataifa.
-
Spika Qalibaf: Daima tunafuatilia kupanua uhusiano na nchi za Afrika
Dec 14, 2025 03:41Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, daima taifa hili limekuwa likifuatilia kupanua ushirikiano na mataifa ya Kiafrika.
-
Brigedia Jenerali Ali Jahanshahi: Iran imejiandaa kukabiliana na aina yoyote ile ya vitisho
Dec 14, 2025 03:40Brigedia Jenerali Ali Jahanshahi, Kamanda wa vikosi vya nchi kavu vya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, vikosi vya ulinzi vikiwa na zana kamili, silaha na uwezo viko tayari kukabiliana na tishio lolote la adui kwa kusikiliza amri ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu.
-
Pezeshkian: BRICS inatoa fursa ya ushirikiano imara zaidi wa wanachama
Dec 13, 2025 23:23Rais Masoud Pezeshkian wa Iran ameashiria nafasi na uwezo wa kundi la BRICS na kulieleza kama jukwaa muhimu la kuimarisha maingiliano na uhusiano wa kiuchumi na kisiasa miongoni mwa nchi wanachama.
-
Khatibzadeh: Uhusiano wa Iran na China mkamilishaji wa mfumo mpya wa kimataifa
Dec 13, 2025 08:11Saeed Khatibzadeh, Naibu Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran na Mkuu wa Kituo cha Utafiti wa Kisiasa na Kimataifa ameutaja uhusiano wa Iran na China uliojengeka juu ya msingi wa chaguo la maslahi ya pamoja.