-
Mtaalamu Mkuu wa UN:Maafisa wa EU washtakiwe kwa ushiriki wao katika jinai za kivita za Israel
May 04, 2025 08:04Mtaalamu mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Palestina ametoa wito wa kutaka maafisa waandamizi wa Umoja wa Ulaya (EU), akiwemo Rais wa Tume ya Ulaya Ursula von der Leyen na Mwakilishi Mkuu wa EU wa Masuala ya Kigeni na Sera ya Usalama Kaja Kallas, wafikishwe mahakamani kwa ushiriki wao katika uhalifu wa kivita unaofanywa na Israel huko Gaza.
-
Mashambulizi dhidi ya Meli ya Uhuru; Jinai nyingine ya Israel
May 04, 2025 06:13Utawala wa Kizayuni wa Israel umefanya jinai nyingine ya kushambulia kwa droni na ndege zisizo na rubani meli za uhuru (Freedom Flotilla) iliyokuwa inapeleka misaada ya kibinadamu kwa wananchi madhlumu wa Ghaza, na hivyo kuzidisha orodha ya jinai za utawala huo katili dhidi ya ubinadamu.
-
Yemen Yapiga marufuku usafirishaji wa mafuta ghafi ya Marekani kupitia Bahari Nyekundu
May 03, 2025 22:58Serikali ya Yemen imetangaza marufuku ya jumla dhidi ya mafuta ghafi ya Marekani, kama jibu kwa mashambulizi yanayoendelea ya Washington kwenye ardhi ya nchi hiyo ya Kiarabu, pamoja na mashambulizi yanayolenga raia na miundombinu ya kiraia.
-
Mjumbe wa UN asema mashambulizi ya anga ya Israel dhidi ya Syria lazima yakome ‘mara moja’
May 03, 2025 22:56Mjumbe Maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Syria, Geir Pedersen, amelaani vikali ukiukaji unaozidi kuongezeka wa mamlaka ya Syria unaofanywa na utawala wa Israel, akisema utawala huo ghasibu lazima usitishe mashambulizi yake ya anga “mara moja.”
-
UNICEF: Watoto wa Gaza wanazidi kujongewa na njaa, maradhi na mauti
May 03, 2025 08:11Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limeonya kwamba watoto katika Ukanda wa Gaza wanakabiliwa na hatari kubwa ya njaa, magonjwa na vifo, miezi miwili baada ya kukabiliwa na mzingiro wa Israel.
-
Qamati: Ni upuuzi na maneno matupu kutaka Hizbullah ipokonywe silaha
May 03, 2025 08:08Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon imesema kuwa, adui ana hofu kubwa na silaha za muqawama na kwamba, ni maneno ya kipuuzi na yasiyo na maana kutaka harakati hiyo ipokonywe silaha.
-
Khatibu wa msikiti wa al-Aqswa aonya kuhusu siasa hatarishi za wavamizi
May 03, 2025 07:44Khatibu wa Msikiti wa Al-Aqswa ameonya kuhusiana na kushadidi mashambulizi ya Wazayuni dhidi ya Msikiti wa Al-Aqswa na Baytul Muqaddas, na na kutoa mwito wa kukabiliana mara moja na vitendo hivyo visivyo vya kibinadamu.
-
Israel yafanya mashambulio 20 dhidi ya Syria, makali zaidi kushuhudiwa tangu ulipoanza mwaka 2025
May 03, 2025 03:26Duru za habari zimeripoti kuwa, usiku wa kuamkia leo, utawala wa Kizayuni wa Israel umefanya mashambulio yasiyopungua 20 ya anga dhidi ya viunga vya mji mkuu wa Syria Damascus, Dara’a, na Hama yakiwa ndio makali zaidi dhidi ya nchi hiyo tangu ulipoanza mwaka huu wa 2025.
-
Israel yaendeleza mauaji ya kikatili Ukanda wa Ghaza, Yemen yapiga tena
May 02, 2025 22:54Takwimu rasmi zinaonesha kuwa, raia 12 wa Palestina wameuawa shahidi katika mashambulizi ya kikatili ya Wazayuni kwenye maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Ghaza hususan katikati mwa ukanda huo. Ukatili huo ulianzia usiku wa manane jana na kuendelea mpaka asubuhi.
-
Lieberman: Kamwe hatuwezi kupata amani Israel
May 02, 2025 22:47Mkuu wa chama cha "Yisrael Beiteinu" amesema kuwa, maadamu utawala unafanya maafa uko madarakani huko Israel, walowezi wa Kizayuni kamwe hawatoonja maisha ya usalama na amani.