-
Ben Gvir alitaka jeshi la Israel litumie 'nguvu kamili' Gaza
May 30, 2025 22:52Waziri wa usalama wa ndani wa utawala wa Kizayuni wa Israel mwenye misimamo ya kufurutu ada, Itamar Ben Gvir ametoa wito wa kutumiwa "nguvu kamili" huko Gaza, baada ya madai ya uongo kwamba Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imepinga pendekezo jipya la Marekani kuhusu usitishaji vita.
-
Ireland yasisitiza Israel inatekeleza mauaji ya kimbari Gaza
May 30, 2025 04:04Katika mjadala mkali uliotikisa bunge la Ireland, naibu waziri mkuu Simon Harris, ametetea msimamo wa serikali kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel unatekeleza mauaji ya kimbari dhidi ya Wapalestina huko Gaza.
-
Mkuu wa UNRWA: Waarabu wawape Wapalestina sehemu ndogo ya Matrilioni waliyompa Trump
May 30, 2025 04:03Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa Linalowahudumia Wakimbizi wa Kipalestina (UNRWA) amezitaka nchi za Kiarabu katika Ghuba ya Uajemi kutenga sehemu ndogo tu ya fedha zilizotajwa katika ‘makubaliano makubwa’ kati yao na Rais wa Marekani, Donald Trump, ili kusaidia wakimbizi wa Kipalestina wanaopambana kuendelea kuishi katika ardhi zao ambazo Israel imezikalia kwa mabavu na pia wale wanaoishi katika nchi jirani.
-
Vikosi vya Yemen vyashambulia uwanja wa ndege Israel kwa kombora la kasi ya juu
May 29, 2025 23:38Vikosi vya kijeshi vya Yemen vimeendesha operesheni nyingine dhidi ya utawala dhalimu wa Israel, kwa kulenga Uwanja wa Ndege wa Ben Gurion kwa kombora la kasi ya juu (hypersonic) ikiwa ni jibu kwa mashambulizi ambayo Israel inaendeleza dhidi ya Wapalestina huko Gaza.
-
Je, utawala wa Trump unataka kubadilisha kisiasa mazingira ya vyuo vikuu vya Marekani?
May 29, 2025 23:35Kutokana na hali ya mvutano inayoendelea kati ya utawala wa Rais Donald Trump wa Marekani na Chuo Kikuu cha Harvard, serikali imetaka kufutwa kwa kandarasi zote za kifedha na chuo hicho.
-
Ni jinai gani nyingine imebakia haijafanywa na Israel
May 29, 2025 23:33Maafa ya kibinadamu huko Ghaza Palestina yamefika kileleni kiasi kwamba katika uhalifu wa karibuni zaidi wa Israel, jeshi katili la utawala wa Kizeyuni limeshambulia vituo vya usambazaji chakula ambavyo Israel yenyewe ilikubali viwepo na mpaka iliainisha viwekwe maeneo gani.
-
Saudia, Qatar, UAE zamuonya Trump asithubutu kuanzisha vita na Iran
May 29, 2025 23:32Tovuti ya habari ya Axios ya Marekani imeripoti kuwa, viongozi wa Saudi Arabia, Qatar, na Imarati (UAE) walipinga vikali shambulizi lolote dhidi ya Iran wakati walipoonana na Trump na kuonya juu ya madhara yake yasiyotabirika kwa washirika wa Marekani kwenye eneo hilo.
-
Siku 600 za mauaji ya kimbari Gaza, Israel yaendeleza jinai
May 29, 2025 06:32Tangu kuanza kwa mashambulizi makubwa ya utawala wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza mnamo Oktoba 2023, hadi Jumatano tarehe 28 Mei 2025, ikiwa ni siku ya 600 ya vita, maisha ya kiraia katika eneo hilo yameporomoka kabisa chini ya mashambulizi yasiyokoma ya Wazayuni.
-
Ansarullah ya Yemen: Kuendelea jinai za Israel Gaza kutazidisha mashambulizi dhidi yake
May 29, 2025 03:44Katibu Mkuu wa Harakati ya Ansarullah ya Yemen ameuonya utawala wa Kizayuni na kuutaka usitishe hujuma na jinai zake dhidi ya Ukanda wa Gaza vinginevyo utaendelea kuandamwa na mashambulio.
-
Hamas yaafiki pendekezo la US la kuondoka askari wote wa Israel Gaza
May 29, 2025 02:37Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imesema imefikia makubaliano na Mjumbe Maalum wa Marekani katika eneo la Asia Magharibi, Steve Witkoff kuhusu "mfumo jumla" wa kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza.