-
Ndege za kivita za Marekani zashambulia Yemen karibu mara 30 katika muda wa chini ya siku moja
Apr 08, 2025 06:47Marekani imefanya karibu mashambulizi 30 ya anga katika majimbo kadhaa kote nchini Yemen katika muda wa chini ya siku moja, na kushadidisha uchokozi wake dhidi ya taifa hilo, katika kile ambacho wataalamu wamekitaja kuwa ni harakati za kujishinda yenyewe za kusitisha bila mafanikio operesheni za Sana'a zinazotekelezwa dhidi ya Israel na waungaji mkono wake kwa ajilii ya kuwatetea wananchi wanaodhulumiwa wa Palestina.
-
Mashirika sita ya UN: Vita vya Ghaza ni ishara ya kutojaliwa hata chembe maisha ya binadamu
Apr 08, 2025 06:21Wakuu wa mashirika sita ya Umoja wa Mataifa wametoa indhari kali kuhusu hali ya Ukanda wa Ghaza na kutaka usitishaji vita utekelezwe tena na kwa haraka sana, huku hali ya kibinadamu ikizidi kuwa mbaya katika eneo hilo linaloendelea kuandamwa na mashambulio ya kinyama ya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Msemaji wa Taliban: Askari wa Marekani hawawezi kuruhusiwa kuwepo ndani ya ardhi ya Afghanistan
Apr 08, 2025 06:11Msemaji wa serikali ya muda ya Afghanistan amesisitiza kuwa haiwezekani askari wa Marekani waruhusiwe kwenda na kuwepo ndani ya ardhi ya nchi hiyo.
-
Waisraeli waandamana kupinga kuanza tena vita vya Gaza
Apr 08, 2025 03:11Maelfu ya waandamanaji wamejitokeza katika mitaa ya Tel Aviv kushiriki katika maandamano mapya ya kupinga serikali ya utawala haramu wa Israel, wakati ambapo Waziri Mkuu, Benjamin Netanyahu alipokutana na Rais wa Marekani, Donald Trump mjini Washington.
-
Watoto laki 6 wa Kipalestina Gaza katika hatari ya kupata ulemavu
Apr 07, 2025 08:06Wizara ya Afya katika Ukanda wa Gaza imesema hatua ya Israel ya kuzuia kampeni ya chanjo ya ugonjwa wa kupooza wa polio inawaweka malaki ya watoto wa Kipalestina katika hatari ya kupata ulemavu wa kudumu.
-
Hamas yapongeza wafanyakazi Microsoft kwa kufichua ushiriki wa kampuni hiyo katika mauaji ya kimbari Gaza
Apr 06, 2025 23:16Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, imeelezea kufurahishwa na misimamo ya baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya Microsoft wakati wa sherehe ya miaka 50 ya kampuni hiyo ya teknolojia wakipinga ushiriki wa Microsoft katika vita vya mauaji ya halaiki vya jeshi la Israeli katika Ukanda wa Gaza.
-
Kusimama imara muqawama wa Yemen kumeleta mabadiliko yapi Asia Magharibi?
Apr 06, 2025 23:14Vikosi vya ulinzi vya Yemen vinaendelea kutekeleza oparesheni katika Bahari Nyekundu na katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina (Israel); na hatua za muqawama wa Yemen zimekuwa na taathira kwa matukio ya kanda hiyo ya Magharibi mwa Asia.
-
Israel 'yaumbuka' baada ya vidio kufichua ukweli halisi kuhusu mauaji ya wahudumu 15 wa tiba
Apr 06, 2025 03:15Vidio iliyopatikana kwenye simu ya mfanyakazi wa Kipalestina wa huduma za tiba aliyeuawa shahidi pamoja na wenzake 14 huko Ghaza mwezi uliopita, inasuta na kukinzana na madai yaliyotolewa na jeshi la utawala haramu wa Kizayuni wa Israel kuhusu namna mauaji ya wahudumu hao yalivyotokea.
-
UNICEF: Watoto zaidi ya milioni moja Ghaza wamekosa misaada kwa zaidi ya mwezi mmoja
Apr 06, 2025 03:11Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF limesema, watoto wa Ukanda Ghaza wanakabiliwa na upungufu mkubwa wa misaada ya kibinadamu wakati huu ambapo utawala ghasibu wa Israel umezuia kikamilifu misaada yote ya kibinadamu ya kuokoa maisha kuingizwa katika eneo hilo.
-
Ripoti: Ukatili unaoendelezwa na Israel Gaza umepita aina zote za ugaidi wa kisasa
Apr 05, 2025 22:59Shirika la Haki za Binadamu la Euro-Med, lenye makao yake mjini Geneva, limelaani vikali ukatili wa Israel katika Ukanda wa Gaza, likisema kuwa ukatili huo "umepita hata aina zote za ugaidi wa kisasa."