-
Wakati anatumikia kifungo jela, Imran Khan ateuliwa kuwania Tuzo ya Amani ya Nobel
Apr 02, 2025 07:01Waziri Mkuu wa zamani wa Pakistani Imran Khan aliyefungwa jela, ameteuliwa kuwania Tuzo ya Amani ya Nobel kwa "kazi aliyofanya kuhusiana na haki za binadamu na demokrasia nchini Pakistan". Hayo yameelezwa katika tamko lililotolewa na chama cha siasa cha Norway Partiet Sentrum.
-
Wapalestina 11 wauawa shahidi katika mashambulizi ya leo ya jeshi la Israel
Apr 02, 2025 03:28Duru za kitiba zimetangaza kuwa Wapalestina 11 wameuawa shahidi katika mashambulizi ya anga ya jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza mapema leo.
-
Hamas: Kila anayeweza ashike silaha kukabiliana na njama ya Trump kuhusu Gaza
Apr 01, 2025 23:35Mjumbe wa ngazi za juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amesema akizungumzia mpango wa Rais Donald Trump wa Marekani wa kuwaondoa Wapalestina Ukanda wa Gaza kwamba: "Mtu yeyote anayeweza kushika silaha anapaswa kuchukua hatua katika uwanja huu."
-
Mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Yemen, je, Marekani itaweza kufungua njia za Bahari Nyekundu?
Apr 01, 2025 11:57Wiki hii, Jeshi la Yemen lilitangaza kuhusika na mfululizo wa mashambulizi yaliyofanyika kwa ustadi wa hali ya juu na kuzitwanga meli za kivita za Marekani, ikiwa ni pamoja na mwanuwari ya USS Harry S. Truman ya Marekani ya kubebea ndege, katika Bahari Nyekundu.
-
Watoto zaidi ya 300 wameuawa katika mashambulizi mapya ya Israel Gaza
Apr 01, 2025 07:08Mamia ya watoto wa Kipalestina wameuawa shahidi tangu utawala wa Kizayuni wa Israel uanze tena operesheni za kijeshi katika Ukanda wa Gaza.
-
Watu watatu wauawa katika hujuma ya Israel jijini Beirut licha ya mapatano ya kusitisha vita
Apr 01, 2025 04:14Katika ukiukaji wa wazi wa makubaliano dhaifu ya kusitisha mapigano kati ya Israel na Lebanon, jeshi la utawala wa Israel limefanya shambulizi dhidi ya jengo la makazi katika kitongoji cha kusini mwa mji mkuu wa Beirut, na kusababisha vifo vya watu wasiopungua watatu na kujeruhi wengine kadhaa.
-
Mpasuko Israel, Smotrich ajiondoa katika utawala wa Netanyahu
Apr 01, 2025 04:12Waziri wa Fedha wa utawala haramu wa Israel, Bezalel Smotrich, ametangaza kujiuzulu kutoka wadhifa wake, jambo ambalo linaongeza matatizo ndani ya serikali ya muungano ya Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu.
-
Jeshi la Yemen laangusha ndege ya kivita ya Marekani aina ya MQ-9
Mar 31, 2025 23:37Jeshi la Yemen limetangaza kuangusha ndege ya kivita ya isiyo na rubani au droni ya Marekani aina ya MQ-9 katika Mkoa wa Ma’rib, ikiwa ni droni ya 16 kuangushwa na nchi hiyo tangu Oktoba 7, 2023.
-
ICRC: Tumeshtushwa na jinsi Israel inavyofanya jinai bila ya kiwewe
Mar 31, 2025 23:18Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu (ICRC) limesema kuwa, limeshtushwa na jinsi utawala wa Kizayuni wa Israel unavyofanya jinai za kutisha huko Ghaza bila ya hofu wala kiwewe.
-
Iran yasisitizia kuharakishwa utekelezaji wa makubaliano kati yake na Qatar
Mar 31, 2025 23:17Rais Masoud Pezeshkian wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo ya simu na Amir wa Qatar na kutilia mkazo wajibu wa kuharakishwa utekelezaji wa makubaliano kati ya nchi hizo mbili na kuimarishwa uhusiano wa kirafiki na ujirani mwema.