-
HAMAS: Uvunjeni mzingiro, komesheni mauaji na hitimisheni kuteswa Wapalestina kwa njaa
Mar 25, 2025 08:53Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa taarifa ya kulaani "mauaji ya kutisha" yanayoendelea kufanywa na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel na kuitolea mwito Jamii ya Kimataifa ichukue hatua za kuudhibiti utawala huo dhalimu.
-
Mazungumzo ya kusitisha vita tena Ghaza yagonga mwamba kwa ukwamishaji wa Israel
Mar 25, 2025 08:51Duru za kuaminika zimefichua kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel umekataa mapendekezo yote yaliyotolewa na wapatanishi ya kusitisha mapigano kutokana na uungaji mkono kamili unaopata kwa Marekani na kwamba mazungumzo juu ya suala hilo yameishia kwenye mkwamo.
-
Mtengeneza filamu mashuhuri ya Palestina iliyoshinda Oscar apigwa na kukamatwa na askari wa Israel
Mar 25, 2025 08:17Hamdan Ballal, mtengeneza filamu mwenza wa Kipalestina wa filamu iliyoshinda tuzo ya Oscar iitwayo Hakuna Ardhi Nyingine (No Other Land) amekamatwa na wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu baada ya kupigwa na kujeruhiwa vibaya sana na walowezi wa Kizayuni. Hayo yameripotiwa na Yuval Abraham aliyeshirikiana naye kutengeneza filamu hiyo.
-
Uwanja wa Ndege wa Israel, manuwari ya Marekani zapigwa kwa makombora
Mar 25, 2025 03:16Msemaji wa jeshi la Yemen ametangaza habari ya kufanyika mashambulizi ya mafanikio dhidi ya Uwanja wa Ndege wa Ben Gurion huko Tel Aviv, mji mkuu wa wa utawala wa Kizayuni na pia dhidi ya manuwari ya kubeba ndege ya Harry Truman ya Marekani kwenye Bahari Nyekundu.
-
HAMAS haitokwama kwa kuuliwa shahidi viongozi wake
Mar 25, 2025 03:16Kiongozi mmoja wa ngazi za juu wa Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina Hamas amesema kuwa, عtawala wa Kizayuni unajidanganya unapodhani kwamba utaweza kuiangamiza Hamas kwa kuwaua shahidi makamanda wake.
-
UNRWA: Mzingiro wa Israel utasababisha baa kubwa la njaa Gaza
Mar 25, 2025 02:53Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Wakimbizi wa Palestina (UNRWA) ametahadharisha kwamba hatua ya utawala wa Israel ya kuweka mzingiro na kuzuia misaada ya kibinadamu kuingia katika Ukanda wa Gaza inapelekea eneo hilo la pwani kukaribia baa kubwa la njaa.
-
Jeshi katili la Israel laendelea kumwaga damu za Wapalestina Gaza
Mar 24, 2025 23:21Wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel wamewaua shahidi Wapalestina wengine 17 katika mashambulizi ya alfajiri ya leo katika Ukanda wa Gaza, siku moja baada ya kuua shahidi Wapalestina zaidi ya 60 akiwemo ripota wa Al Jazeera, Hossam Shabat katika ukanda huo.
-
Umuhimu wa msimamo wa kamati ya mawaziri wa nchi za Kiarabu na Kiislamu dhidi ya jinai za utawala wa Kizayuni huko Ghaza.
Mar 24, 2025 22:49Kamati ya Mawaziri ya Nchi za Kiarabu na Kiislamu imeelezea wasi wasi wake kuhusu mashambulizi mapya ya utawala wa Kizayuni katika Ukanda wa Gaza na kutaka kutekelezwa mara moja na kikamilifu usitishaji vita kwa mujibu wa azimio nambari 2735 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Chombo cha Kizayuni: Kuna ukosefu wa kuaminiana kitaasisi Israel
Mar 24, 2025 07:22Chombo kimoja cha habari cha lugha ya Kiebrania kimechapisha makala inayofichua mzozo mkubwa wa kutoaminiana ndani ya muundo wa mamlaka na kiutawala huko Israel.
-
Siku ya saba ya uvamizi wa Israel wa Ghaza; makumi wauawa na kujeruhiwa
Mar 24, 2025 07:21Utawala wa wa Kizayuni wa Israel Israel unaendelea kufanya jinai na mashambulizi ya anga katika maeneo mbalimbali ya Ukanda wa Ghaza ambapo tangu asubuhi ya leo hadi wakati tunaandaa taarifa hii, makumi ya Wapalestina wamekuwa wameshauwa shahidi na kujeruhiwa, leo ikiwa ni siku ya saba ya tangu kuanza wimbi jipya la jinai za utawala wa Kizayuni huko Ghaza.