-
HAMAS yasitisha mchakato wa kuwaachia mateka kutokana na Israel kukiuka makubaliano ya kusitisha vita
Feb 11, 2025 03:44Brigedi za Izzuddinul-Qassam, tawi la kijeshi la Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS zimetangaza kuwa, zinasitisha mchakato wa kuwaachia huru mateka wa Israel uliopangwa kutekelezwa Jumamosi ijayo hadi litakapotolewa tangazo jengine, kutokana na utawala wa Kizayuni kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano katika Ukanda wa Ghaza.
-
Ratiba ya wakati na mahali yatapofanyika mazishi ya Shahidi Nasrullah na Shahidi Safiyyuddin yatangazwa
Feb 11, 2025 03:44Kamati ya vyombo vya habari inayohusika na shughuli ya mazishi ya Katibu Mkuu na Mkuu wa Baraza la Kisiasa la Hizbullah ya Lebanon waliouawa shahidi imetangaza kuwa shughuli ya mazishi hayo itafanyika siku ya Jumapili, Februari 19 saa saba mchana.
-
Juhudi za Trump za kufutililia mbali mpango wa kuundwa nchi huru ya Palestina
Feb 10, 2025 12:00Kuongezeka misaada ya silaha ya Rais Donald Trump wa Marekani kwa Israel pamoja na mpango wake wa kuwahamisha kwa nguvu wakazi wa Ukanda wa Gaza na kuwapeleka Misri na Jordan kunaonyesha kuwa moja ya vipaumbele vyake ni kubadili ramani ya eneo hilo na kuharibu kabisa mpango wa kuanzisha nchi huru ya Palestina.
-
Arab League yalaani wazo la Netanyahu la kuwahamishia Wapalestina Saudia
Feb 10, 2025 07:56Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu amelaani vikali matamshi yaliyotolewa na Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, ambaye alipendekeza kuwa Saudi Arabia inaweza kuunda taifa la Palestina ndani ya ardhi yake.
-
Ben-Gvir: Israel imegeuzwa kuwa 'kioja' Mashariki ya Kati
Feb 10, 2025 07:55Aliyekuwa waziri wa usalama wa ndani wa Israel, Itamar Ben-Gvir amesema utawala huo wa Kizayuni umekuwa kioja na kichekesho katika eneo la Asia Magharibi.
-
Wanajeshi wa Israel wamuua mwanamke mjamzito wa Kipalestina na kichanga chake katika Ukingo wa Magharibi
Feb 09, 2025 23:13Wanajeshi wa Israel wamemuua kwa kumpiga risasi mwanamke Mpalestina aliyekuwa na ujauzito wa miezi minane na kichanga kilichokuwa tumboni mwake wakati askari jeshi wa utawala huo ghasibu walipovamia kambi ya wakimbizi ya Nur Shams kaskazini magharibi mwa Ukingo wa Magharibi unaokaliwa kwa mabavu.
-
Duru ya Kizayuni: Netanyahu anajaribu kuvuruga makubaliano ya kusitisha mapigano Gaza
Feb 09, 2025 23:12Chombo kimoja cha bahari cha lugha ya Kiibrania kimetangaza kuwa Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel anafanya kila awezalo kuvuruga makubaliano ya kusimamisha mapigano katika Ukanda wa Gaza.
-
Wakimbizi wa Palestina waendelea kutumia eneo la Netzarim baada ya Israel kuondoka kikamilifu
Feb 09, 2025 07:11Vyombo mbalimbali vya habari vimetangaza kuwa, baada ya wanajeshi wa Israel kutoka kwenye eneo la Netzarim huko Ghaza kama yalivyosema makubaliano ya kusimamisha vita, hivi sasa wakimbizi wa Palestina wanaendelea kuvuka eneo hilo na kurejea kwenye maeneo yao.
-
Saudia yajibu kwa kauli kali matamshi ya kijuba ya Netanyahu kuhusu Palestina
Feb 09, 2025 07:09Wizara ya Mambo ya Nje ya Saudi Arabia imepongeza upinzani wa kimataifa dhidi ya matamshi ya kijuba ya waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu kuhusiana na Ukanda wa Ghaza na imepinga hatua yoyote ya kuhamishwa Wapalestina kutoka kwenye ardhi zao.
-
Lebanon yaunda serikali ya kwanza baada ya zaidi ya miaka miwili
Feb 09, 2025 03:39Lebanon imeunda serikali yake ya kwanza kamili tangu mwaka 2022, wakati huu ambapo nchi hiyo ya Kiarabu inajitahidi kujenga upya eneo lake la kusini lililoharibiwa na vita; na kuhakikisha usalama unarejea baada ya mapigano kati ya Israel na Harakati ya Muqawama ya Hizbullah.