-
Jeshi la Yemen laangusha ndege nyingine ya kivita ya Marekani aina ya MQ-9
Jan 01, 2025 23:11Vikosi vya ulinzi wa anga vya Yemeni vimefanikiwa kudungua tena ndege nyingine ya kivita isiyo na rubani ya Marekani aina ya MQ-9 Reaper wakati ilipokuwa ikifanya shughuli za uhasama katika anga la mkoa wa katikati-magharibi wa Ma'rib.
-
NGO: Israel inashikilia miili ya Wapalestina 198 waliouawa mwaka 2024
Jan 01, 2025 09:32Kampeni ya Kitaifa ya Kurejesha Miili ya Mashahidi (The National Campaign to Retrieve Martyrs' Bodies) imeeleza kuwa viongozi wa utawala ghasibu wa Israel wanashikilia miiili ya mashahidi wa Kipalestina 198 walisajiliwa mwaka jana wa 2024.
-
Utawala wa Kizayuni unaharibu mazingira kusini mwa Lebanon
Jan 01, 2025 08:57Jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limeanza kuharibu mazingira ya kusini mwa Lebanon kabla ya kumalizika muhula wa usitishaji vita kati ya utawala huo ghasibu na Lebanon.
-
Himaya ya wananchi katika Ulimwengu wa Kiislamu kwa muqawama wa Palestina
Jan 01, 2025 04:08Mwaka mpya wa Miladia wa 2025 umeanza katika ulimwengu wa Kiislamu kwa himaya na uungaji mkono mkubwa wa wananchi kwa makundi ya wapiganaji wa Palestina na viongozi wa muqawama.
-
Shahid Sinwar ndiye mtu maarufu zaidi wa Ulimwengu wa Kiarabu mwaka 2024
Jan 01, 2025 03:12Wazungumzaji wa lugha ya Kiarabu ulimwenguni wamemchagua shahidi Yahya Sinwar, kiongozi wa kisiasa wa Hamas, kuwa mtu maarufu zaidi wa Ulimwengu wa Kiarabu kwa mwaka 2024.
-
Ghaza yaanza Mwaka Mpya kwa kushambuliwa kikatili na Israel
Jan 01, 2025 03:09Katika dakika za awali kabisa za kuingia Mwaka Mpya wa 2025, jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel limefanya mashambulizi mengine ya kinyama kwenye Ukanda wa Ghaza kutoka kaskazini hadi kusini mwa ukanda huo uliozingirwa kila upande.
-
Wizara ya Elimu: Wanafunzi 12,943 wameuawa shahidi tangu Israel ianzishe vita Gaza
Jan 01, 2025 00:17Wizara ya Malezi na Mafunzo ya Juu ya Palestina imetangaza kuwa, zaidi ya wanafunzi 12,000 wameuawa shahidi tangu jeshi la utawala haramu wa Israel lilipoanzisha hujuma na mauajii yan kimbari katika Ukanda wa Gaza Oktoba mwaka juzi 2023.
-
Matarajio yetu ni kuuawa shahidi; Majibu ya Ansarullah ya Yemen kwa orodha ya magaidi wa Israel
Jan 01, 2025 00:10Mwanachama mmoja wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amezungumzia hatua ya kuchapishwa orodha ya walengwa wa mashambulizi ya kigaidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel kusema: "Hatumuogopi yeyote isipokuwa Mwenyezi Mungu, na tunamuomba atuondoe duniani kwa njia ya kuuliwa shahidi."
-
Hamas: Wapalestina wanakufa kwa baridi kali Ukanda wa Gaza; yaitaka UN ichukue hatua
Jan 01, 2025 00:09Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) imeitolea wito jamii ya kimataifa na Umoja wa Mataifa kuchukua hatua hivi sasa ambapo raia wa Palestina wanaaga dunia kwa baridi kali huko Gaza huku Israel ikiendeleza mauaji ya kimbari dhidi ya wakazi wa eneo hilo.
-
Jeshi la Yemen laushambulia uwanja wa Ndege wa Ben Gurion wa Israel na kituo cha umeme
Jan 01, 2025 00:09Vikosi vya ulinzi vya Yemen vimetangaza kuhusika na msururu wa operesheni dhidi ya maeneo kadhaa ya Israel na Marekani katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu katika kuwaunga mkono wananchi wa Palestina wa Ukanda wa Gaza na kujibu mashambulizi ya Marekani na Uingereza dhidi ya Yemen.