-
Kuongezeka harakati za kundi la al-Qaeda nchini Afghanistan
Sep 03, 2024 23:04Katika ripoti yake, jarida la Foreign Policy limedai kuwa, baada ya kundi la Taliban kutwaa tena udhibiti na madaraka nchini Afghanistan, nyayo na ishara za kundi la kigaidi la Al-Qaeda zinazidi kuonekana na kupanuka katika nchi hiyo. Jarida la Foreign Policy linasema, hilo linatokana na kuwa kundi la Taliban halifanyi juhudi kubwa kwa minajili ya kuyakandamiza makundi ya kigaidi, na hili linasababisha kupanuka wigo wa harakati za makundi kama al-Qaeda nchini Afghanistan.
-
Jumuiya ya MSF yailaumu Israel kwa uharibifu unaoendelea mkabala wa mlipuko wa polio huko Gaza
Sep 03, 2024 08:05Kundi la Misaada la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) linalojulikana pia kama Jumuiya ya Madaktari Wasio na Mipaka limesisitiza kuwa mashambulizi ya Israel na kuharibiwa miundo mbinu ya Ukanda wa Gaza ndio uliosababisha mlipuko wa polio katika eneo hilo.
-
Takwa la Al-Azhar la kususiwa bidhaa za utawala wa Kizayuni
Sep 03, 2024 05:17Chuo Kikuu cha Kiislamu cha al Azhar cha Misri kimelaani jinai zinazofanywa na Wazayuni dhidi ya wananchi wa Palestina na kutoa wito kwa Waislamu kususia bidhaa zinazotengenezwa na utawala wa Kizayuni.
-
HAMAS: Netanyahu ameshindwa kufanikisha lengo lolote zaidi ya mauaji ya kizazi
Sep 03, 2024 03:16Harakati ya Mapambano ya Kisilamu ya Palestina HAMAS imesema leo Jumanne kwamba, Benjamin Netanyahu, waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni anawadanganya wafuasi wake na serikali ya Marekani anapodai kupata ushindi katika vita vya Ghaza kwani hajafanikisha lengo hata moja zaidi ya kuua kwa umati na kikatili watu wasio na hatia.
-
HAMAS yaangamiza na kujeruhi wanajeshi wengine wa Israel katika mtego kabambe
Sep 02, 2024 07:33Brigedi za Izzuddin al Qassam, Tawi la Kijeshi la Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Kiislamu ya Palestina HAMAS imeonesha namna iliyoweka mtego kabambe katika mji wa Jenin kaskazini mwa Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan na kuangamiza na kujeruhi wanajeshi kadhaa wa utawala wa Kizayuni.
-
Brigedi za Al-Qassam: Netanyahu amehusika na mauaji ya mateka wa Israel
Sep 02, 2024 03:47Tawi la kijeshi wa harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) limetoa ujumbe wa video ulioelekezwa kwa familia za mateka wa Israel wanaoshikiliwia huko Gaza ukisisitiza kuwa Netanyahu amehusika na mauaji ya mateka wa Israel katika eneo la Ukanda wa Gaza.
-
Netanyahu katika kinamasi cha mivutano na mizozo ya ndani
Sep 01, 2024 23:35Hali ya wasiwasi na mgogoro wa ndani ya Tel Aviv vimezidi kupamba moto kutokana na ongezeko la maandamano katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina (Israel) na kuongezeka hitilafu kati ya Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni, Benjamin Netanyahu, na wapinzani wake.
-
Netanyahu asema, atawatoa kafara mateka Waisraeli lakini jeshi la Kizayuni libaki Philadelphi
Sep 01, 2024 06:45Waziri Mkuu mshupalia vita wa utawala wa Kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu amemueleza waziri wake wa vita Yoav Gallant kwamba anafadhilisha jeshi la Israel libaki kwenye Ukanda wa Philadelphi (Mhimili wa Saladin) kuliko kuokoa maisha ya mateka ambao wangali wanashikiliwa katika Ukanda wa Ghaza.
-
Waisraeli 3 waangamizwa katika operesheni ya kulipiza kisasi karibu na al-Khalil
Sep 01, 2024 03:10Kwa uchache askari polisi wawili wa Israel na mlowezi mmoja wa Kizayuni wameangamizwa katika operesheni ya kulipiza kisasi karibu na mji wa al-Khalil, katika eneo la Palestina la Ukingo wa Magharibi.
-
Wazayuni wazidi "kumkalia kooni" nduli wa Ghaza
Aug 31, 2024 22:51Matokeo ya uchunguzi wa karibuni kabisa wa maoni uliofanywa na Kanali ya 12 ya televisheni ya Israel yanaonesha kuwa, walowezi wengi wa Kizayuni wanaoishi katika ardhi za Palestina zilizopachikwa jina bandia la Israel, wanachukizwa sana na kuendelea Benjamin Netanyahu kung'ang'ania kuwa waziri mkuu wa utawala huo.