-
Erdogan: Naweza kuonana na Rais Bashar Assad wa Syria wakati wowote kutokea sasa
Jul 08, 2024 00:09Rais Recep Tayyip Erdogan wa Uturuki ametoa ishara mpya ya kuanzisha tena uhusiano kati yake na serikali ya Syria kwa kutangaza kuwa huenda karibuni hivi akatuma mwaliko kwa Rais Bashar al-Assad wa kutembelea Uturuki.
-
Hamas yakadhibisha madai ya kutumia shule za UNRWA huko Gaza
Jul 07, 2024 08:57Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina, Hamas, imesema kuwa madai yaliyotolewa na utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuwepo wapiganaji wake katika shule ya Al-Jaouni katika kambi ya wakimbizi ya Nuseirat ya Ukanda wa Gaza ni ya uongo na ya upotoshaji.
-
Hizbullah kwa Pezeshkian: Tutakuwa pamoja kwenye njia ya Muqawama hadi 'ushindi wa mwisho'
Jul 07, 2024 08:56Harakati ya Hizbullah ya Lebanon imempongeza rais mteule wa Irani, Masoud Pezeshkian, kwa ushindi wake, na kuahidi kwamba harakati hiyo itaendelea kuwa katika njia ya Muqawama wa Kiislamu pamoja na serikali ya Jamhuri ya Kiislamu chini ya uongozi wa rais mteule.
-
Walowezi wa Kizayuni wachoma moto mashamba ya Wapalestina huko Ramallah
Jul 07, 2024 04:36Walowezi wa Kizayuni ambao kwa miaka mingi wanakalia kwa mabavu ardhi za Wapalestina wameteketeza moto sehemu kubwa ya mashamba ya Wapalestina kaskazini mwa Ramallah.
-
Wanahabari 5 ni miongoni mwa Wapalestina 29 waliouawa Gaza
Jul 06, 2024 07:50Wizara ya Afya ya Ukanda wa Gaza imesema waandishi wa habari watano ni miongoni mwa Wapalestina 29 waliouawa shahidi ndani ya saa 24 zilizopita na wanajeshi makatili wa Israel katika eneo hilo la Palestina linalokaliwa kwa mabavu na utawala wa Kizayuni.
-
Jibu kali na indhari ya mara kwa mara ya Wamagharibi kuhusu chokochoko dhidi ya Hizbullah
Jul 06, 2024 05:47Sambamba na jibu kali la Hizbullah ya Lebanon kwa operesheni za kigaidi za utawala wa Kizayuni wa Israel huko Lebanon, vyanzo vya Magharibi vinaendelea kutahadharisha kuhusu matokeo ya chokochoko za kijeshi za Waziri Mkuu Benjamin Netanyahu kwa kueleza uwezo wa kijeshi wa Hizbullah.
-
Hizbullah ya Lebanon yalenga makao ya kuongoza operesheni za kijeshi za Utawala wa Kizayuni
Jul 06, 2024 03:08Hizbullah ya Lebanon ililenga makao makuu ya kamandi ya Kitengo cha 91 cha utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Israel yaendelea kumwaga damu za Wapalestina Jenin, Jabalia
Jul 05, 2024 23:07Wakazi watano wa mji wa Jenin ni miongoni mwa makumi ya Wapalestina waliouawa shahidi kwa kupigwa risasi na kushambuliwa kwa mabomu na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel katika maeneo mbali mbali ya Palestina jana Ijumaa.
-
Hali si hali Israel; Kamanda Mzayuni: Tuko tayari kusimamisha vita Ghaza kwa gharama yoyote
Jul 05, 2024 06:52Huku baadhi ya duru za utawala wa Kizayuni zikisema kwamba, matumaini ya kufikiwa makubaliano ya kusimamisha vita na HAMAS yameongezeka, jeshi lililochoka la Israel limetangaza kuwa liko tayari kukubali kusimamisha vita kwa gharama yoyote ile.
-
Al Houthi: Manuwari zinazobeba ndege za kivita za Marekani ni mfumo wa kizamani wa silaha ya vita
Jul 05, 2024 04:00Kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen amevipongeza vikosi vya wanamaji vya nchi hiyo kwa operesheni za baharini dhidi ya meli zenye uhusiano na Israel katika Bahari Nyekundu.