-
Uhispania, Ireland na Norway zaitambua rasmi Palestina
May 29, 2024 00:17Uhispania, Ireland na Norway jana zilipasisha rasmi mpango wa kutambua rasmi Palestina, katika uamuzi ulioratibiwa hatua ambayo imeongeza himaya na uungaji mkono kwa Palestina barani Ulaya.
-
Kiongozi wa kidini wa Iraq ataka ubalozi wa Marekani ufungwe kufuatia shambulio la Israel Rafah
May 29, 2024 00:09Moqtada Sadr, Kiongozi wa kidini wa Iraq mwenye ushawishi amerudia wito wake wa kutaka ubalozi wa Marekani mjini Baghdad ufungwe baada ya shambulizi la anga lililofanywa na jeshi la utawala wa Kizayuni wa Israel kuwaua makumi ya raia wa Palestina katika eneo lililodaiwa kuwa na usalama katika mji wa Rafah kusini mwa Ukanda wa Ghaza.
-
Israel kuwekewa vikwazo na Umoja wa Ulaya kutokana na jinai zake Rafah
May 28, 2024 07:14Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Ireland amesema kuwa, kwa mara ya kwanza Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Umoja wa Ulaya wamejadili kwa kina uwezekano wa kuuwekea vikwazo utawala wa Kizayuni iwapo hautatekeleza amri ya Mahakama ya Kimataifa ya Haki (ICJ) ya kusimamisha mashambulizi ya kijeshi dhidi ya Rafah.
-
Waandamanaji wachoma moto ubalozi mdogo wa Israel mjini Istanbul
May 28, 2024 07:12Ubalozi mdogo wa utawala wa Kizayuni wa Israel mjini Istanbul Uturuki umechomwa moto na waandamanaji wenye hasira waliokuwa wakilalamikia vita na mauaji yanayofanywa na utawala haramu wa Israel dhidi ya wananchi wa Palestina katika ukanda wa Gaza.
-
Uhispania: Kutambuliwa rasmi Palestina ni haki ya kisheria ya taifa hilo madhulumu
May 28, 2024 07:11Waziri Mkuu wa Uhispania amesema kuwa, kutambuliwa rasmi Palestina ni haki ya kisheria ya taifa hilo madhulumu.
-
Harakati za muqawama wa Palestina: Hatutashiriki katika mazungumzo yoyote na utawala wa Kizayuni
May 28, 2024 04:37Harakati za Mapambano za Palestina za Hamas na Jihadul Islami zimetangaza kuwa hazitashiriki tena kwenye mazungumzo yoyote baada ya utawala wa Kizayuni kushambulia kambi ya wakimbizi wa Kiaplestina katika mji wa Rafah.
-
Azma ya dhati ya Iran na Saudi ya kudumisha na kuimarisha ushirikiano
May 27, 2024 23:20Saudi Arabia ikiwa na lengo la kutoa heshima na mkono wa pole kwa taifa na wananchi wa Iran kufuatia kufa shahidi Rais Ebrahim Raisi ilituma hapa mjini Tehran ujumbe uliokuwa ukiongozwa na mjumbe maalumu wa Mfalme wa nchi hiyo sambamba na Waziri wa Mashauri ya kigeni wa nchi hiyo.
-
Imarati yaalani jinai za utawala wa Kizayuni katika mji wa Rafah
May 27, 2024 23:15Wizara ya Mambo ya Nje ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) imelaani jinai za utawala wa kizayuni katika mji wa Rafah kusini mwa Ukanda wa Gaza na kusisitiza kuwa kuna udharura utawala wa Kizayuni kufungamana na maamuzi ya Mahakama ya Kimataifa ya ICJ.
-
MSF wawasilisha kesi mpya ICC dhidi ya utawala wa Kizayuni kwa mauaji ya waandishi habari Gaza
May 27, 2024 23:14Jumuiya ya Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) imewasilisha mashtaka mapya katika mahakama ya kKimataifa ya Jinai (ICC) kufuatia jinai za kivita za utawala wa Kizayuni dhidi ya waandishi wa habari katika Ukanda wa Gaza.
-
Amnesty International yaitaka mahakama ya ICC kuchunguza jinai za Israel Rafah
May 27, 2024 08:27Shirika la Msamaha Duniani la Amnesty International limeitaka Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kuchunguza jinai zinazofanywa na utawala wa Kizayuni katika mji wa Rafah katika Ukanda wa Gaza.