-
Katibu Mkuu wa UN: Ni 35% tu ya malengo ya SDG yanaelekea kufikiwa ifikapo 2030
Jul 16, 2025 03:25Ni asilimia 35 tu ya malengo ya maendeleo endelevu yanakaribia kufikia malengo yao ifikapo mwaka 2030. Hayo yameelezwa na Umoja wa Mataifa katika ripoti yake mpya.
-
Russia yatoa mjibizo kwa muhula wa siku 50 iliopewa na Trump
Jul 16, 2025 03:14Msemaji wa Kremlin, Dmitry Peskov amesema, Russia inahitaji muda kutathmini kitisho alichotoa Rais wa Marekani Donald Trump cha kuwawekea vikwazo vikali washirika wa kibiashara wa Moscow ikiwa mzozo wa Ukraine hautatatuliwa ndani ya siku 50.
-
Rais Maduro alaani kimya cha walimwengu kwa mauaji ya kimbari ya Israel dhidi ya Wapalestina
Jul 15, 2025 23:47Rais Nicolas Maduro wa Venezuela amekosoa vikali kimya cha walimwengu mbele ya mauaji ya kimbari ya Wapalestina yanayofanywa na utawala wa Kizayuni na kusisitiza haki ya muqawama (mapambano) na kuwepo taifa la Palestina.
-
Uchunguzi wa maoni: Wajapani hawako tayari kuisamehe Marekani
Jul 15, 2025 07:35Matokeo ya uchunguzi mpya wa maoni nchini Japan unaonyesha kuwa, nusu ya manusura wa mlipuko wa bomu la atomiki nchini humo "hawawezi" kuisamehe Marekani kwa shambulio la bomu la atomiki nchini Japan.
-
New York Times: Marekani ililipua kituo cha kuwazuilia wahamiaji wa Kiafrika Yemen
Jul 15, 2025 07:23Gazeti la New York Times limekiri kuhusika moja kwa moja na kwa kimakusudi Marekani katika kulenga kituo cha wahamiaji wa Kiafrika katika Mkoa wa Saada mwishoni mwa mwezi Aprili mwaka huu.
-
Ripoti: Zaidi ya watoto milioni 14 hawakuchanjwa 2024
Jul 15, 2025 07:19Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, zaidi ya watoto milioni 14 hawakupata chanjo kabisa mwaka jana (2024).
-
US yaweka rekodi mpya ya kuogofya, yatimua maelfu ya watoto
Jul 15, 2025 01:13Zaidi ya watoto 8,300 wahamiaji wasio na vibali, wenye chini ya umri wa miaka 11 walipewa maagizo ya kufukuzwa nchini Marekani mwezi Aprili, hiyo ikiwa ni idadi ya juu zaidi ya kila mwezi kuwahi kurekodiwa nchini humo.
-
Wananchi wa Argentina waandamana kuliunga mkono taifa la Palestina
Jul 14, 2025 09:51Maandamano makubwa yamefanyika katika mji mkuu wa Argentina, Buenos Aires, huku maelfu ya wananchi wakikusanyika katika baadhi ya barabara kuu na nembo na vituo muhimu vya jiji hilo, kutangaza himaya na uungaji mkono wao kwa taifa madhulumu la Palestina.
-
Kupungua uungaji mkono wa wafuasi wa MAGA kwa vita vya Israel dhidi ya Iran; sababu, matokeo na athari zake kwa siasa za Marekani
Jul 14, 2025 05:41Katika miezi ya hivi karibuni, anga ya kisiasa ya Marekani imeshuhudia mabadiliko makubwa katika mtazamo wa wafuasi wa MAGA yenye maana ya Ifanye Tena Kuu Marekani, (Make America Great Again) kuhusiana na vita vya Israel dhidi ya Iran.
-
Karibu 50% ya Wajapan manusura wa bomu la nyuklia wasema "hawawezi kuisamehe" Marekani
Jul 14, 2025 03:02Uchunguzi uliofanywa na Shirika la Habari la Kyodo la Japan unaonyesha kuwa, karibu asilimia 70 ya manusura wa shambulio la bomu la atomiki lililofanywa na Marekani dhidi ya nchi hiyo wanaamini kuwa silaha za nyuklia zinaweza kutumika tena.