-
US yamwekea vikwazo ripota wa UN Albanese kwa kukosoa jinai za Ghaza
Jul 10, 2025 02:49Marekani imetangaza kuwa inamwekea vikwazo ripota maalumu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Palestina, Francesca Albanese.
-
Borrell amkemea Netanyahu kwa kutaka Trump apewe Tuzo ya Amani ya Nobel
Jul 10, 2025 02:39Mkuu wa zamani wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya Josep Borrell amekemea pendekezo la waziri mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu la kutaka rais wa Marekani Donald Trump atunukiwe Tuzo ya Amani ya Nobel, akilielezea hilo kuwa ni hatua iliyochukuliwa na "mtu anayeaminika kuwa mhalifu wa kivita" kwa ajili ya "muuzaji wake mkuu wa silaha".
-
Kwa nini watu wengi duniani wana mtazamo hasi kuhusu Marekani?
Jul 09, 2025 23:19Kwa mujibu wa uchunguzi wa maoni uliochapishwa na Kituo cha Utafiti cha Pew, watu wa Canada na Mexico, majirani wawili wa karibu wa Marekani, wanaitambua nchi hiyo kuwa tishio kubwa zaidi kwao.
-
Bunge la Ujerumani latilia shaka uhalali wa mashambulizi ya US, Israel dhidi ya Iran
Jul 09, 2025 14:56Huenda mashambulio ya Israel na Marekani dhidi ya vituo vya nyuklia vya Iran mwezi uliopita yalikiuka sheria za kimataifa, kwa mujibu wa ripoti ya wataalamu wa bunge la Ujerumani iliyonukuliwa na shirika la habari la dpa.
-
Grossi: Uwezo wa nyuklia wa Iran hauwezi kuzimwa kwa mabavu
Jul 09, 2025 12:26Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati wa Atomiki IAEA amesema kuwa, mpango wa nyuklia wa Iran, nchi yenye uwezo mkubwa wa kiuchumi, kiviwanda na kiteknolojia hauwezi kuzimwa kwa hatua za kijeshi wala hatua zozote za mabavu.
-
Wanazuoni 100 wa Kiislamu wawatangaza Trump na Netanyahu kuwa maadui wa Mwenyezi Mungu
Jul 09, 2025 10:59Kundi la wanazuoni na wasomi 100 wa Kiislamu kutoka sehemu mbalimbali duniani wametoa tamko rasmi wakimtangaza Rais wa Marekani Donald Trump na Waziri Mkuu wa utawala haramu wa Israel Benjamin Netanyahu kuwa maadui wanaopigana na Mwenyezi Mungu, na ni waharibifu katika ardhi.
-
Seneta, mbunge wa US walaani mhalifu wa vita Netanyahu kukaribishwa tena White House
Jul 09, 2025 04:43Seneta wa Marekani Bernie Sanders na Mbunge Ilhan Omar wamelaani waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu kukaribishwa tena mjini Washington na katika Ikulu ya White House wakati utawala huo ghasibu unaendeleza vita vya kinyama na mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Gaza, ambapo zaidi ya Wapalestina 57,500 wameuawa shahidi hadi sasa.
-
Waislamu Uholanzi wamtimua Imamu aliyeimba wimbo wa taifa wa Israel mbele ya Herzog
Jul 09, 2025 04:30Imamu wa Msikiti wa Bilal nchini Uholanzi Youssef Msibih amesimamishwa kazi na uongozi wa msikiti huo baada ya kukutana na rais wa utawala wa kizayuni wa Israel Isaac Herzog kama sehemu ya ujumbe wa Waislamu kutoka Ulaya wanaotembelea Israel.
-
Kwa mara ya kwanza, Mahakama ya Uhispania yachunguza jinai za Netanyahu na wenzake
Jul 08, 2025 12:34Mahakama ya Taifa ya Uhispania imeanzisha uchunguzi wa uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu anaoshutumiwa kuufanya waziri mkuu wa utawala wa kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu, waziri wake wa vita Israel Katz, na maafisa kadhaa waandamizi wa jeshi la utawala huo haramu hususan shambulio la mwezi uliopita lililofanywa jeshi la kizayuni dhidi ya meli ya misaada ya kibinadamu.
-
Trump na Netanyahu wajadili kuwahamisha Wapalestina kwa nguvu Ghaza
Jul 08, 2025 12:29Waziri mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel Benjamin Netanyahu amekutana na Rais wa Marekani Donald Trump katika Ikulu ya White House, huku viongozi hao wawili wakirudia pendekezo lao tata la kuwahamisha kwa nguvu maelfu ya Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza.