-
Waandamanaji Stockholm walaani mashambulizi ya Israel dhidi ya Gaza licha ya usitishaji vita
Jan 25, 2026 11:12Wananchi wa Sweden wamefanya maandamano mengine katika mji mkuu wa nchi hiyo, Stockholm, kulaani mashambulizi ya Israel yanayowalenga Wapalestina katika Ukanda wa Gaza licha ya kufikiwa mapatano ya usitishaji vita.
-
Maandamano yashtadi US baada ya raia mwingine kuuawa Minneapolis
Jan 25, 2026 06:59Maajenti wa serikali kuu ya Marekani wamemuua kwa kumpiga risasi mtu mwingine mjini Minneapolis huku kukiwa na msako mkali dhidi ya wahamiaji, na kushadidisha maandamano na wito mpya kwa Rais Donald Trump kuwaondoa mara moja maafisa hao waliojizatiti kwa silaha katika jiji hilo lililoko katika jimbo la Minnesota.
-
Trump aitishia Canada kwa ushuru wa 100%, kisa biashara na China
Jan 25, 2026 06:57Rais wa Marekani, Donald Trump ametishia kuitoza Canada ushuru wa asilimia 100 iwapo Waziri Mkuu wa Canada, Mark Carney atatekeleza makubaliano ya kibiashara na China.
-
Kwa nini Baraza la Haki za Kibinadamu la UN, linaichafua Iran, sambamba na Marekani?
Jan 24, 2026 13:36Baraza la Haki za Kibinadamu la Umoja wa Mataifa limefuata sera ya Marekani ya kuichafua Iran kwa kupasisha azimio dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu.
-
Venezuela: Marekani ilitufanya panya wa maabara katika shambulio la kumteka nyara Maduro
Jan 24, 2026 12:57Waziri wa Ulinzi wa Venezuela amethibitisha kwamba Marekani ilitumia silaha zisizojulikana wakati wa shambulizi la kumteka nyara Rais Nicolas Maduro wa nchi hiyo.
-
Iran yalaani kikao cha UNHRC, yasema haitasalimu amri mbele ya mashinikizo ya kigeni
Jan 24, 2026 07:55Iran siku ya Ijumaa ilipinga kikao maalum cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa (UNHRC), ikikitaja kuwa hakina uhalali. Mjumbe wa Iran mjini Geneva alisisitiza kwamba Iran halijawahi na halitakubali kutawaliwa au kushinikizwa na nguvu za kigeni.
-
Uchunguzi wa maoni waonyesha wengi Ulaya wanamwona Trump kama ‘adui’ kuliko ‘rafiki
Jan 24, 2026 07:55Uchunguzi mpya wa maoni umebaini kwamba katika baadhi ya nchi kubwa barani Ulaya, watu wengi zaidi wanamwona rais wa Marekani kama “adui” kuliko “rafiki” au mshirika wa Ulaya.
-
Starmer amtaka Trump aombe radhi kwa kauli ya 'kutusi' aliyotoa kuhusu uvamizi wa Afghanistan
Jan 24, 2026 03:31Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer ametaka Rais wa Marekani Donald Trump aombe radhi kwa madai yake kwamba wanajeshi wa Ulaya hawakuwa mstari wa mbele katika vita vya kivamizi vya mwaka 2001 vilivyoanzishwa na Marekani na waitifaki wake dhidi ya Afghanistan.
-
Orban: Hungary haitaruhusu Ukraine kujiunga na EU miaka 100 ijayo
Jan 24, 2026 02:47Waziri Mkuu wa Hungary, Viktor Orban amesema kwamba Ukraine inajaribu kushawishi na kuathiri matokeo ya uchaguzi ujao wa bunge nchini Hungary, akisitiza kuwa nchi yake haitaruhusu Ukraine kujiunga na Umoja wa Ulaya katika miaka 100 ijayo.
-
Kwa nini rais wa Brazil amemkejeli Trump?
Jan 24, 2026 02:47Rais Lula da Silva wa Brazil amemkejeli Rais Donald Trump wa Marekani kutokana na tweet nyingi za kutatanisha anazoandika katika mitandao ya kijamii.