-
Khan: Uingereza ilitishia kukata ufadhili wa ICC kutokana na waranti wa kukamatwa Netanyahu
Dec 12, 2025 06:54Mwendesha Mashtaka wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC), Karim Khan, amesema serikali ya Uingereza ilitishia kuikatia mahakama hiyo ufadhili na kujiondoa kwenye Mkataba wa Roma uliounda taasisi hiyo, endapo jopo la majaji lingeendelea na mpango wa kutoa waranti wa kukamatwa kwa waziri mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu.
-
Iran yakosoa kupunguzwa misaada ya kimataifa kwa wakimbizi wa Afghanistan
Dec 12, 2025 02:38Iran imeikosoa jamii ya kimataifa kwa kushindwa kutimiza hata ahadi za kimsingi za kuwasaidia mamilioni ya wakimbizi wa Kiaghani; ikisema kuwa kupunguzwa misaada kumeifanya nchi hiyo kubeba mzigo mkubwa wa kifedha licha ya indhari za miaka mingi.
-
Mashtaka ya ICC dhidi ya Trump: Jinamizi kwa Ikulu ya White House?
Dec 12, 2025 02:36Ikulu ya Rais wa Marekani, White House, ina wasiwasi kuhusu uwezekano wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai (ICC) kutoa kibali cha mashtaka dhidi ya Donald Trump.
-
Marekani yatwaa meli ya mafuta ya Venezuela katika wizi na uharamia wa wazi
Dec 11, 2025 11:33Marekani imeshadidisha ghadhabu za walimwengu baada ya kutwaa meli ya mafuta ya Venezuela katika kile kilichotajwa na serikali ya Caracas kuwa hatua inayoshabihiana na uvamizi wa kijeshi wa Israel ulio kinyume cha sheria. Caracas iimekemea hatua hiyo ikiitaja kuwa ni "uharamia wa kimataifa."
-
Kwa kuhofia Trump asije akafuatiliwa, White House yatoa vitisho, yaitaka ICC iifanyie mabadiliko hati yake
Dec 11, 2025 06:10Shirika la habari la Reuters limezinukuu duru za kuaminika na kuripoti kuwa, serikali ya Marekani imewasiliana kwa siri na Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC na kutishia kuiwekea vikwazo vipya ikiwa itajaribu kumshtaki Rais wa Marekani Donald Trump kwa uwezekano wa kuhusika na uhalifu.
-
Ripoti: Asilimia 10 ya watu duniani wanamiliki asilimia 75 ya utajiri wa dunia
Dec 11, 2025 03:33Ripoti iliyotolewa na The Global Economic Inequality (GEI) kuhusu ukosefu wa usawa wa kiuchumi duniani imeonya pengo linaloongezeka kati ya matajiri na maskini na haja ya dharura la kushughulikia mgogoro huu, ikisema: asilimia 10 ya idadi ya watu duniani wanamiliki asilimia 75 ya utajiri wote wa dunia.
-
Namna mfumo wa Ubepari unavyowatumia wanawake kama nyenzo tu
Dec 11, 2025 02:37Mfumo wa Ubepari umekuwa siku zote ukiwatumia wanawake kama nyenzo tu za kuuwezesha kupata faida zaidi.
-
Marekani yachunguza vifo vinavyoshukiwa kuhusishwa na chanjo za virusi vya corona
Dec 10, 2025 10:15Wizara ya Afya na Huduma za Kibinadamu ya Marekani imetangaza kwamba Idara ya Chakula na Dawa (FDA) inafanya uchunguzi wa kina kuhusu vifo vinavyoweza kuhusishwa na chanjo za COVID-19, vinavyohusisha makundi mengi ya umri.
-
Ripoti ya Ujerumani: Waislamu na watu weusi wanasumbuliwa na ubaguzi wa kimfumo
Dec 10, 2025 06:20Ripoti ya Shirika la Kitaifa la Uchunguzi wa Ubaguzi la serikali ya Ujerumani imefichua kwamba Waislamu na watu weusi wanaoishi nchini humo wanasumbuliwa na "ubaguzi wa kimfumo" kuhusu hali ya makazi.
-
RSF: Israel ni muuaji mkuu wa waandishi wa habari duniani
Dec 10, 2025 02:41Shirika la Waandishi wa Habari Bila Mipaka (RSF) limesema utawala wa Israel ni muuaji mkuu wa waandishi wa habari duniani kwa mwaka wa tatu mfululizo, na limeutaka utawala huo uwajibike kwa kusababisha karibu nusu ya vifo vya waandishi wa habari duniani mwaka 2025, hasa katika Ukanda wa Gaza unaozingirwa.