Libya yaialika Italia katika maji yake kupambana na magendo ya binadamu
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i32302-libya_yaialika_italia_katika_maji_yake_kupambana_na_magendo_ya_binadamu
Serikali ya Libya yenye makao yake huko Tripoli mji mkuu wa nchi hiyo imezialika meli za kivita za Italia katika maji ya nchi hiyo ili kusaidia mapambano dhidi ya magendo ya binadamu. Hayo yamesemwa leo na Paolo Gentiloni Waziri Mkuu wa Italia.
(last modified 2023-11-27T12:14:11+00:00 )
Jul 26, 2017 14:06 UTC
  • Libya yaialika Italia katika maji yake kupambana na magendo ya binadamu

Serikali ya Libya yenye makao yake huko Tripoli mji mkuu wa nchi hiyo imezialika meli za kivita za Italia katika maji ya nchi hiyo ili kusaidia mapambano dhidi ya magendo ya binadamu. Hayo yamesemwa leo na Paolo Gentiloni Waziri Mkuu wa Italia.

Awali Fayez al Sarraj Waziri Mkuu wa Libya anayeongoza serikali ya Libya inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa yenye makao yake huko Tripoli alipinga kuwepo katika maji ya nchi hiyo kikosi cha Umoja wa Ulaya cha kupambana na magendo ya binadamu kwa jina la "Sophia" na hivyo kukwamisha jitihada za kukomesha biashara hiyo tangu kuanza kutekelezwa mwaka 2015.

Paolo Gentiloni Waziri Mkuu wa Italia katika mazungumzo na mwenzake wa Libya Fayez al Sarraj katika Ikulu ya Chigi mjini Roma

Hata hivyo Waziri Mkuu huyo wa Libya baadaye alibadilisha msimamo wake siku moja baada ya kufikiwa makubaliano kati yake na Khalifa Haftar kamanda anayesimamia eneo la mashariki mwa Libya ya kusimamisha vita kwa masharti ya kuendesha uchaguzi mwakani. Waziri Mkuu wa Italia amesema kuwa siku kadhaa zilizopita Waziri Mkuu wa Libya Fayez al Sarraj alimtumia barua akiiomba serikali ya Roma iwapatie msaada wa kiufundi katika juhudi za pamoja za kupambana na magendo ya binadamu.