Zoezi la kuwarejesha nyumbani wakimbizi wa Rwanda kutoka DRC laanza +SAUTI
Nov 18, 2020 13:40 UTC
Serikali ya Rwanda imeanza zoezi la kuzihamishia familia 1800 ambazo kwa takribani mwaka mzima ziliishi kwenye kambi ya muda magharibi mwa Rwanda baada ya kurejea kutoka misitu ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Rwanda inasema kwa mwaka mzima raia hao wamekuwa wakipewa mafunzo ya uraia mwema hivyo wananchi hawa hawana budi kuishi vema na ndugu zao huko uraiani.
Kutoka Kigali mwandishi wetu Sylivanus Karemera anaripoti zaidi