-
Kuwa tayari Iran kuimarisha ushirikiano na nchi za eneo
Apr 04, 2025 06:57Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amefanya mazungumzo kwa njia ya simu na wakuu wa baadhi ya nchi za eneo na kusisitiza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko tayari kuimarisha uhusiano na ushirikiano na nchi hizo katika nyanja mbalimbali kwa mujibu wa imani na itikadi za Kiislamu.
-
Kwa nini mashambulizi ya Marekani dhidi ya Wayemen hayana athari?
Apr 03, 2025 23:05Kanali ya 12 ya Televisheni ya Utawala wa Kizayuni imekiri kuwa mashambulizi ya Marekani dhidi ya Yemen hayajazaa matunda. Licha ya mashambulizi hayo kuongezeka, hayakuweza kuzuia mashambulizi ya makombora yanayoelekezwa Israel.
-
Onyo Kali la Iran kwa Marekani na Utawala wa Kizayuni
Apr 03, 2025 09:08Katika mazingira ya kuongezeka kwa vita vya kisaikolojia vinavyoendeshwa na Marekani pamoja na utawala wa Kizayuni, na vitisho vya mara kwa mara kutoka kwa Donald Trump na maafisa waandamizi wa usalama wa utawala wake huko Washington kuhusu uwezekano wa kushambulia Iran iwapo kutakosekana makubaliano kuhusu suala la nyuklia, Tehran imetoa onyo kali kwa Marekani na Israel kuhusu madhara makubwa ya hatua yoyote ya kijeshi dhidi ya Iran.
-
Muungano wa makundi ya Muqawama wa kukabiliana na njama za utawala wa Kizayuni
Apr 02, 2025 23:00Viongozi wa makundi ya Muqawama katika eneo la Asia Magharibi wametoa ujumbe kwa nyakati tofauti wakisisitiza kwamba wataendelea kukabiliana na njama za utawala wa Kizayuni kwa umoja wao.
-
Marekani inapokosa mwamana; Trump atishia kuiteka kijeshi Greenland
Apr 02, 2025 09:13Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa ana yakini eneo la Greenland la Denmark kwa vyovyote vile litatekwa na kukaliwa na Marekani hata kama ni kwa kutumia nguvu za kijeshi.
-
Vipaumbele vya Afrika wakati wa uenyekiti wa Afrika Kusini ndani ya G20
Apr 02, 2025 00:05Wataalamu na watunga sera waliohudhuria mkutano kuhusu vipaumbele vya Afŕika wakati wa Urais wa Afrika Kusini wa Kundi G20 wamesisitizia haja ya kuyapa kipaumbele mageuzi muhimu ambayo yatasaidia ustawi na maendeleo ya Afŕika na kutumiwa vizuri utajiri mkubwa wa rasilimali wa bara hilo.
-
Mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Yemen, je, Marekani itaweza kufungua njia za Bahari Nyekundu?
Apr 01, 2025 11:57Wiki hii, Jeshi la Yemen lilitangaza kuhusika na mfululizo wa mashambulizi yaliyofanyika kwa ustadi wa hali ya juu na kuzitwanga meli za kivita za Marekani, ikiwa ni pamoja na mwanuwari ya USS Harry S. Truman ya Marekani ya kubebea ndege, katika Bahari Nyekundu.
-
Ukatili wa Polisi Dhidi ya Waandamanaji wa Siku ya Kimataifa Quds Nchini Nigeria
Mar 31, 2025 23:09Katika maandamano ya Siku ya Kimataifa ya Quds yaliyofanyika nchini Nigeria Ijumaa kwa kushirikisha mamia ya Waislamu na wanachama wa Harakati ya Kiislamu ya nchi hiyo – kwa lengo la kuonyesha mshikamano na watu wa Palestina na kulaani uhalifu wa utawala wa Kizayuni wa Israel– maafisa wa polisi wa Nigeria walifyatua risasi dhidi ya waandamanaji. Tukio hilo lilisababisha waandamanaji wasiopungua 18 kuuawa shahidi, wengine kujeruhiwa, na wengi kukamatwa.
-
Utawala wa Kizayuni waendelea kupinga utoaji wa misaada kwa Wapalestina
Mar 31, 2025 06:43Vitendo vya kikatili vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Wapalestina wanaoishi Gaza vinaendelea, na bado utawala huo unazuia kufikishwa kwa misaada ya chakula na dawa kwa wakazi wa Gaza.
-
Marekani, Mshirika Asiyeaminika
Mar 30, 2025 23:09Waziri Mkuu wa Canada, Mark Carney, ambaye amemrithi Justin Trudeau, amesisitiza kwamba atajibu hatua za Marekani dhidi ya nchi hiyo katika nyanja za kiuchumi na kibiashara, na amekiri kwamba: "Marekani si mshirika wa kuaminika tena."