Jenerali Ashtari: Maadui wa Iran ya Kiislamu wameshindwa kwa fedheha
Mkuu wa Jeshi la Polisi la Iran amesisitiza juu ya ulazima wa kuegemea Jihadi ya ufafanuzi na kuweka wazi mambo katika vita vya simulizii na akasema: "Maadui wa Iran ya Kiislamu wameshindwa kwa fedheha katika makabiliano yao na wananchi."
Brigedia Jenerali Hossein Ashtari, Kamanda Mkuu wa Jeshi la Polisi la Iran, Jumamosi akizungumzia fitna za hivi karibuni humu nchini amesema: "Maadui wanataka kufikia malengo yake ya kutisha na yaliyofichika katika hali yoyote ile ili kwa njia hiyo kudhuru usalama na utulivu wa wananchi na kutekeleza mpango wao wa kupindua mfumo mtakatifu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran."
Katika sehemu nyingine ya hotuba yake, Jenerali Ashtari, akizungumzia njama za hivi karibuni za maadui na watu wasioutakia mema mfumo wa Kiislamu, zikilenga zaidi vita mseto na operesheni za kisaikolojia, amesema: "Jeshi la polisi limesimama pamoja na wananchi katika uwanja wa mapambano ili kulinda na kutetea usalama na wananchi na hivyo njama za maadui zimeambulia patupu."
Mkuu wa Jeshi la Polisi la Iran amebainisha kuwa: "Adui ameingia kwa nguvu zake zote na kuleta kila alichonacho uwanjani ili tusiwe na Iran yenye nguvu na huru, adui anataka kuchochea tofauti za kikabila, kidini na kujitenga maeneo ya nchi, lakini ameshindwa kwa fedheha kubwa."