-
Tarehe 16 Azar; Nembo ya utamaduni wa muqawama na harakati ya uhuru
Dec 08, 2025 07:31Tarehe 16 mwezi Azar inayosadifiana na Disemba 7 imesajiliwa katika kalenda rasmi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwa ni "Siku ya Mwanachuo", siku ambayo ni nembo ya mapambano, kupigania haki na kusimama kidete tabaka la wasomi dhidi ya dhulma na ubeberu wa madola ya kigeni.
-
Araghchi: Marekani haiko tayari kwa mazungumzo ya manufaa kwa pande mbili, ya usawa na ya kuheshimiana
Dec 08, 2025 03:02Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi amesema, Tehran imefikia hitimisho kwamba Marekani haiko tayari kwa mazungumzo ya manufaa kwa pande mbili, ya usawa na yanayofanyika kwa msingi wa kuheshimiana.
-
Iran: Mkakati mpya wa Usalama wa Taifa wa Marekani unaandikwa hasa kwa ajili ya Israel
Dec 07, 2025 23:37Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Mkakati mpya wa Usalama wa Taifa wa Marekani (NSS) unaobainisha misingi na vipaumbele vya Washington katika sera za nje kimsingi ni hati ya usalama kwa ajili ya utawala wa kizayuni wa Israel.
-
Qalibaf azionya nchi jirani kutoijaribu Iran kuhusu visiwa vitatu vya Ghuba ya Uajemi
Dec 07, 2025 07:39Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge la Iran) Mohammad Baqer Qalibaf amepuuzilia mbali madai ya kukaririwa kuhusu visiwa vitatu vya Iran katika taarifa ya mwisho ya Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi (GCC), akiyaonya mataifa jirani kutoijaribu azma ya Jamhuri ya Kiislamu ya kulinda mamlaka yake ya kujitawala na umoja wa ardhi nzima ya nchi hii.
-
Spika Qalibaf: Marekani ina chuki ya kihistoria na mwanachuo wa Kiirani
Dec 07, 2025 03:22Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa: Mfumo wa kibeberu kinara wake akiwa Marekani una chuki na uadui wa kihistoria dhidi ya mwanachuo wa Kiirani.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Hivi sasa mpira uko upande wa Marekani
Dec 07, 2025 03:21Waziri wa Mambo ya Nje wa Ira amesema iwapo Marekani itabadili mkondo wake, Iran nayo itakuwa tayari kupata matokeo ya haki na usawa.
-
Iran, Misri zaafiki kuendeleza mazungumzo ya kupanua uhusiano
Dec 07, 2025 00:11Mawaziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Misri wameafiki juu ya kuweko mazungumzo ya kupanua uhusiano wa mataifa yao.
-
India, Russia zasisitiza utatuzi wa mpango wa nyuklia wa Iran kupitia mazungumzo
Dec 06, 2025 04:24Baada ya Rais wa Russia Vladimir Putin na Waziri Mkuu wa India Narendra Modi kukutana mjini New Delhi, nchi hizo mbili zimesisitiza umuhimu wa kutatua masuala yanayohusiana na mpango wa nyuklia wa Iran kwa njia ya mazungumzo.
-
Je, hatua ya Iran na Uturuki kuelekea ustawi wa eneo inaashiria kufunguliwa ukurasa mpya wa ushirikiano?
Dec 05, 2025 08:18Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki zimeazimia kwa dhati kuchukua hatua kuelekea maendeleo na ustawi wa kikanda.
-
Ayatullah Khatami: Iran haijawahi kuwa na wasomi wengi wanawake kama ilivyo hii leo
Dec 05, 2025 08:03Khatibu wa Swala ya Ijumaa ya leo mjini Tehran amechambua hotuba iliyotolewa siku chache zilizopita na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Ali Khamenei katika hadhara ya wanawake, akielezea mtazamo wa Uislamu kuhusu wanawake, na kusisitiza kwamba Iran haijawahi kuwa na wanawake wengi wasomi na wenye maono kama ilivyo sasa, na jambo hili linaonyesha jinsi utawala wa Kiislamu hapa nchini unavyowathamini wanawake."