-
Kuendelea mgogoro nchini Algeria; kususiwa uchaguzi wa Bunge na vyama vya siasa
Apr 06, 2021 22:04Mgogoro wa kisiasa nchini Algeria ungali unaendelea kufukuta kwani licha ya juhudi za serikali za kutuliza hali ya mambo na kuitisha uchaguzi wa Bunge wa mapema, lakini vyama vinne vya siasa vya nchi hiyo vimetangaza kususia uchaguzi huo.
-
Mtetemeko mkubwa wa ardhi waikumba Algeria mapema leo afajiri
Mar 18, 2021 03:44Mtetemeko mkubwa wa ardhi wenye ukubwa wa daraja 6 kwa kipimo cha rishta umetokea katika eneo la kaskazini mashariki mwa mji wa Bejaia, katika umbali wa kilomita 10 chini ya ardhi huko Algeria.
-
Maandamano yafanyika nchini Algeria kwa wiki ya pili mfululizo
Mar 07, 2021 04:51Maelfu ya raia wa Algeria wamefanya maandamano kwa wiki ya pili mfululizo kulalamikia siasa za serikali ya nchi hiyo.
-
Kuvunjwa Bunge na mwanzo wa kipindi kipya cha kisiasa nchini Algeria
Feb 20, 2021 06:47Katika miaka ya karibuni Algeria imekumbwa na misukosuko na matukio mengi ya kisiasa. Tukio la karibuni kabisa nihatua ya Rais Abdelmadjid Tebboune wa nchi hiyo ya kulivunja Bunge na kuitisha uchaguzi wa mapema. Tebboune alitangaza hatua hiyo Alkhamisi iliyopita katika hotuba yake kwa taifa iliyotolewa kwa mnasaba wa maadhimisho ya Siku ya Taifa ya Shahidi.
-
Bunge la Algeria lavunjwa; rais aitisha uchaguzi
Feb 19, 2021 03:37Rais wa Algeria ameagiza kuvunjwa bunge la nchi hiyo. Rais Abdul Majid Tebboune wa Algeria jana usiku alisema kuwa amelivunja bunge ili kuendesha uchaguzi pasina ufisadi na kuandaa fursa za ajira kwa ajili ya nguvu kazi ya vijana nchini humo.
-
Maelfu ya wapinzani waandamana Algeria kuunga mkono harakati ya Hirak
Feb 17, 2021 04:28Maelfu ya watu waliandamana jana katika mji wa Kherrata nchini Algeria kuunga mkono Harakati ya Hirak ambayo ilimuondoa madarakani rais mkongwe Abduaziz Bouteflika mwaka 2019. Maandamano hayo yalisitishwa baada ya kuanza maambukizi ya COVID-19 mwaka jana.
-
Askari wanne wa jeshi la Tunisia wauawa katika mpaka wa pamoja na Algeria
Feb 04, 2021 00:57Msemaji wa Wizara ya Ulinzi ya Tunisia ametangaza kuwa askari wanne wa jeshi la nchi hiyo wameuawa katika mripuko wa bomu la kutegwa ardhini uliotokea kwenye mpaka wa pamoja wa Tunisia na Algeria.
-
Kukataa kuomba radhi Macron kwa jinai ilizofanya Ufaransa enzi za ukoloni nchini Algeria
Jan 22, 2021 06:55Ufaransa, ambayo ilikuwa moja ya madola ya kikoloni, ina faili chafu na la kuaibisha kuhusiana na uvamizi, ukaliaji ardhi kwa mabavu na vitendo vya jinai ilivyofanya mnamo karne ya 20 katika nchi ilizozikoloni hususan Algeria.
-
Macron: Ufaransa haitaiomba radhi Algeria kwa dhulma za enzi za ukoloni
Jan 21, 2021 00:57Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa amesema nchi hiyo ya Ulaya 'haitatubu' wala kuiomba radhi Algeria kutokana na jinai zilizofanywa na Wafaransa katika zama walipoikoloni nchi hiyo ya Kiafrika.
-
Algeria, nchi ya kwanza Afrika kupasisha chanjo ya corona ya Russia
Jan 11, 2021 04:30Algeria imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika kupasisha chanjo ya COVID-19 iliyotengenezwa nchini Russia.