-
UN yasikitika kufungwa maisha jela viongozi wa upinzani Bahrain
Feb 02, 2019 02:47Umoja wa Mataifa umetilia shaka mchakato wa kesi, baada ya mahakama ya Bahrain kuwahukumu kifungo cha maisha jela viongozi wa upinzani nchini humo.
-
Mkuu wa Baraza la Maulamaa wa Kishia Bahrain atiwa nguvuni tena masaa 24 tangu alipotolewa jela
Jan 31, 2019 14:54Utawala wa Aal Khalifa umemtia nguvuni tena Sheikh Majid Mash'al, mwanazuoni wa Kishia na mkuu wa Baraza la Maulamaa wa Kiislamu wa Bahrain, baada ya kupita masaa 24 tu tangu alipotolewa jela.
-
EU, Amnesty zaikosoa Bahrain kwa kumfunga maisha jela Sheikh Salman
Jan 29, 2019 14:04Umoja wa Ulaya umekosoa vikali hatua ya Mahakama ya Juu ya Bahrain ya kuidhinisha kifungo cha maisha jela dhidi ya shakshia mashuhuri wa kidini na kisiasa nchini humo, Sheikh Ali Salman.
-
Mwaka 2019, mwaka mbaya zaidi kwa haki za binaadamu nchini Bahrain
Jan 21, 2019 01:32Kamati ya watu waliotiwa mbaroni katika Ukanda wa Pwani nchini Bahrain imetangaza kwamba, katika jela ya Jau nchini Bahrain, maafisa usalama wa utawala wa Aal-Khalifa na katika kulipiza kisasi dhidi ya wafungwa wa kesi za uhuru wa kujieleza, wanatekeleza siasa za kuwatesa kwa njaa wafungwa hao.
-
Pembetatu ya kuzua mivutano katika Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi
Jan 19, 2019 03:06Katika ripoti yake ya hivi karibuni, shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema kuwa hali ya haki za binadamu katika nchi tatu za Saudi Arabia, Imarati na Bahrain ni ya kutisha mno.
-
Bahrain yaendelea kukabiliwa na ukandamizaji wa kisiasa wa utawala wa Aal Khalifa
Jan 17, 2019 11:05Utawala wa kiimla wa ukoo wa Aal Khalifa nchini Bahrain umeshadidisha ukandamizaji wake dhidi ya raia wa nchi hiyo katika mwaka huu wa 2019. Katika siku za hivi karibuni kumeshuhudiwa uongezeko la ukandamizaji wa wananchi ambapo wanajeshi wa utawala wa Aal Khalifa wamekandamiza kwa mkono wa chuma maandamano ya amani ya wananchi katika mji wa Al Akr kusini mwa mji mkuu Manama.
-
Kongamano la kulaani jinai za serikali ya Bahrain lafanyika Beirut
Jan 17, 2019 07:44Washiriki wa Kongamano la Kimataifa la kulaani jinai za utawala wa Aal-Khalifa nchini Bahrain wamekosoa kimya cha jamii ya kimataifa mbele ya ukandamizaji wa serikali ya Manama kwa raia wake.
-
Ripoti: Wafungwa wa kisiasa Bahrain wana hali mbaya
Jan 10, 2019 07:14Kituo cha Haki za Binadamu na Demokrasia nchini Bahrain kimetahadharisha kuhusu hali mbaya ya wanaharakati wa kutetea haki za binadamu waliofungwa katika jela za utawala wa Aal Khalifa nchini humo.
-
Sisitizo la Umoja wa Mataifa la kuachiwa huru Nabeel Rajab
Jan 05, 2019 12:55Farhan Haq msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelaani namna utawala wa Aal Khalifa unavyokiuka uhuru wa kiraia huko Bahrain na kutaka kuachiwa huru haraka iwezekanavyo Nabeel Rajab Mkuu wa Kituo cha Haki za Binadamu cha nchini humo.
-
Afungwa miaka mitano jela kwa kusema tu Wayemen wanaonewa
Dec 31, 2018 13:37Ikiwa ni kuendeleza dhulma yake isiyo na kifani, utawala wa kiimla wa ukoo wa Aal Khalifa wa nchini Bahrain umemuhukumu kifungo cha miaka mitano jela, mwanaharakati maarufu Nabil Rajab kwa kuandika tu katika mtandao wa Twitter kwamba Wayemen wanadhulumiwa na muungano vamizi wa Saudi Arabia.