Jun 23, 2022 03:43
Bunge la utawala haramu wa Israel (Knesset) limepiga kura ya kujivunja, na hivyo kuandaa mazingira ya uwezekano wa kurejea madarakani kwa kinara wa chama cha Likud, Benjamin Netanyahu, huku baraza la mawaziri la muungano wa Waziri Mkuu, Naftali Bennett, likiporomoka.