Kikao cha kwanza cha bunge la Lebanon kimefanyika kwa kuchaguliwa Spika na Naibu Spika wa bunge hilo.
Bunge la Iraq limepasisha kwa kauli moja sheria ya kupiga marufuku ya kuanzisha uhusiano wa kawaida na utawala haramu wa Kizayuni wa Israel.
Rais Kais Saied wa Tunisia amelivunja Bunge la nchi hiyo kufuatia kushtadi mivutano ya kisiasa nchini humo.
Rais wa Tunisia, Kais Saied jana Jumatano alitangaza kuvunja Bunge muda mfupi baada ya bunge hilo kupitisha sheria ya kufuta hatua za dharura zilizotangazwa na kiongozi huyo majira ya joto mwaka jana.
Mmoja wa viongozi wa vyama vya upinzani nchini Afrika kusini amekituhumu chama tawala cha Kongresi ya Taifa cha nchi hiyo (ANC) kuwa kimehusika na moto ulioteketeza kikamilifu sehemu ya jengo la Bunge la nchi hiyo.
Kikao cha Bunge la Kenya kimebadilika na kuwa ulingo wa ndondi baada ya wabunge kadhaa kuanza kupigana wakati mjadala ukiendelea kuhusu muswada wa muungano ulioibua mgawanyiko.
Hassan bin Abdullah al Ghanim amechaguliwa kuwa Spika wa kwanza wa Bunge la Qatar baada ya kupigiwa kura 37 za 'ndiyo' na wabunge wa bunge hilo lililoundwa kupitia uchaguzi wa hivi karibuni.
Abdallah Bilhaq Msemaji wa bunge la Libya lenya makao yake katika mji wa Tobruk mashariki mwa nchi hiyo jana adhuhuri alitangaza kuwa bunge hilo limepiga kura ya kutokuwa na imani na serikali ya mpito ya hiyo.
Agizo la kuundwa serikali ya Lebanon limesainiwa rasmi na Rais Michel Aoun wa nchi hiyo.
Licha ya malalamiko ya kila upande, lakini Rais wa Tunisia Kais Saied ametangaza kuwa, shughuli za Bunge la nchi hiyo zitaendelea kusitishwa kwa muda usiojulikana.