-
Tahadhari ya China kuhusu uingiliaji wa nchi za Magharibi katika masuala ya ndani ya nchi nyingine
Jul 07, 2023 23:07Rais wa China, Xi Jinping, ametoa wito kwa nchi mbalimbali kusimama dhidi ya "mapinduzi ya rangi ya nchi za Magharibi". Jinping ametoa wito huo katika mkutano Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai, uliofanyika kwa njia ya mtandao.
-
China yakosoa mauzo mapya ya silaha za Marekani kwa Taiwan
Jul 05, 2023 06:29China imekosoa vikali mpango mpya wa serikali ya Marekani wa kuiuzia Taiwan silaha zenye thamani ya mamilioni ya dola, ikisisitiza kuwa mauzo hayo yanakiuka kanuni ya "China Moja".
-
China: Marekani ituondolee vikwazo iwapo inataka mazungumzo ya kijeshi
Jun 29, 2023 23:54Beijing imesema serikali ya Rais Joe Biden wa Marekani sharti iiondolee China vikwazo iwapo inataka kufanyike mazungumzo ya ngazi ya juu ya kijeshi baina ya madola hayo mawili makubwa.
-
Chokochoko mpya zilizoanzishwa na Biden kuhusiana na China
Jun 22, 2023 22:57Rais Joe Biden wa Marekani siku ya Jumanne wiki hii alimfananisha mwenzake wa China, Xi Jinping na madikteta.
-
China yamshambulia Biden kwa kudai kuwa Rais Xi ni dikteta
Jun 21, 2023 23:04Beijing imekosoa vikali matamshi ya Rais Joe Biden wa Marekani aliyedai kuwa Rais Xi Jingping wa China ni dikteta.
-
Safari ya kwanza ya Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani nchini China baada ya miaka mitano
Jun 19, 2023 09:41Anthony Blinken Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani Jumapili ya jana tarehe 18 Juni aliwasili Beijing mji mkuu wa China, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kupunguza mvutano unaoongezeka kati ya nchi mbili hizo ambao umezitia wasiwasi nchi nyingi.
-
China:Uhusiano wetu na Marekani uko katika kiwango cha chini kabisa
Jun 19, 2023 05:28Mwanadiplomasia wa ngazi ya juu wa China amesema kuwa uhusiano wa nchi hiyo na Marekani umefika katika kiwango cha chini kuwahi kushuhudiwa katika historia na kutahadharisha kuwa hali hiyo haina maslahi kwa nchi yoyote ile.
-
China na Palestina zaafikiana kuanzisha ushirikiano wa kistratajia
Jun 15, 2023 03:04Rais Xi Jinping wa China amekutana na kufanya mazungumzo na Mahmoud Abbas, Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina mjini Beijing, ambapo wawili hao wameafikiana juu ya kuanzisha ushirikiano wa kistratajia.
-
China: Tutaendelea kuunga mkono kadhia ya Palestina
Jun 12, 2023 01:09Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa China amesema Beijing itaendelea kuunga mkono mapambano halali ya Wapalestina ya kupigania haki zao za kitaifa, na kusisitiza kwamba kadhia ya Palestina ni katika masuala muhimu ya eneo la Asia Magharibi.
-
China yaitaka Marekani iache undumakuwili, ulaghai wa kisiasa
Jun 10, 2023 06:53Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya China amesema mtazamo na misimamo ya Marekani mkabala wa mpango wa nyuklia wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ni mfano mwingine wa sera za kindumakuwili za Washington.