Oct 09, 2016 08:08
Ghulam Hussein Dehqani, Balozi na Naibu Mwakilishi wa Iran katika Umoja wa Mataifa siku ya Ijumaa katika kikao cha Kamati ya Tatu ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu dawa za kulevya alisema, zaidi ya asilimia 80 ya ufyuni na zaidi ya asilimia 40 ya heroini inayokamatwa kutoka kwa walanguzi duniani hukampatwa na vikosi vya usalama vya Iran.