-
Trump awaandikia barua viongozi wa nchi za Afrika, adai kuwa "anawaheshimu sana" Waafrika
Jan 28, 2018 00:59Rais Donald Trump wa Marekani amewaandikia barua viongozi wa nchi 55 za Afrika wanaokutana kwenye kikao cha Umoja wa Afrika (AU) mjini Addis Ababa, Ethiopia akisema kuwa "anawaheshimu sana" watu wa bara hilo.
-
Msimamo wa Umoja wa Afrika dhidi ya siasa za chuki na dharau za Trump
Jan 26, 2018 08:27Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika amewataka viongozi wa bara la Afrika kujibu matamshi ya kipumbavu na ya matusi ya Rais wa Marekani dhid ya Waafrika.
-
"Trump ni hatari kwa dunia, yumkini asimalize muhula wake"
Jan 26, 2018 04:32Mwekezaji bilionea mashuhuri wa Marekani, George Soros ameutaja utawala wa Rais Donald Trump kama hatari kwa dunia, na kusisitiza kuwa, kushtadi upinzani dhidi ya kiongozi huyo kutamfanya asahaulike kabisa duniani kufikia mwaka 2020 au hata kabla ya hapo.
-
AU: Afrika haiwezi kunyamazia kimya matusi ya Trump
Jan 26, 2018 03:44Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika amesema bara la Afrika lilishtushwa na lingali linaendelea kutafakari kuhusu kauli chafu na ya kebehi iliyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani, kwamba wahamiaji wanaoingia nchini Marekani kutoka bara hilo, Haiti na El Salvador wanatoka kwenye nchi za "shimo la kinyesi".
-
Sisitizo kwa Umoja wa Ulaya la kujitoa katika makucha ya Marekani
Jan 26, 2018 00:29Kansela wa Ujerumani, Angela Merkel, amesema mbele ya Baraza la Kimataifa la Uchumi mjini Davos Uswisi kwamba nchi za Ulaya zinapaswa kubadilisha siasa zao za kuitegemea Marekani katika masuala ya ndani na nje ya bara hilo.
-
Maelfu ya watu waandamana kupinga safari ya Trump nchini Uswisi
Jan 24, 2018 04:25Maelfu ya raia wa Uswisi wameandamana mjini Zurich na katika miji mingine muhimu ya nchi hiyo ikiwemo ya Geneva, Lausanne na Fribourg kupinga Rais Donald Trump wa Marekani kuhudhuria kongamano la kila mwaka la Jukwaa la Uchumi Duniani (WEF) linalofanyika katika mji wa Davos.
-
Nusu ya Wamarekani wanaamini Trump hana akili timamu
Jan 22, 2018 04:30Matokeo ya uchunguzi mpya wa maoni yanaonyesha kwamba, nusu ya raia wa Marekani wanaamini kwamba, Rais Donald Trump wa nchi hiyo hana mlingano wa akili.
-
Joto lilivunja rekodi duniani mwaka 2017, wasiwasi kuhusu mustakabali
Jan 20, 2018 01:08Mwaka uliopita wa 2017 umetajwa kuwa mwaka uliovunja rekodi ya joto kali zaidi katika historia ya sayari ya dunia pasina kuwepo tukio la El Niño huku kukiwa na wasi wasi kuwa hali itazidi kuwa mbaya katika miaka ijayo.
-
Mkutano wa al-Azhar: Baytul-Muqaddas ni mji mkuu wa milele wa Palestina
Jan 19, 2018 00:44Washiriki wa mkutano wa kimataifa wa kuunga mkono Quds uliofanyika katika Chuo Kikuu cha al-Azhar huko Cairo Misri umesisitiza umuhimu wa kutangazwa Baytul-Muqaddas kuwa mji mkuu wa milele wa Palestina.
-
Abbas: Quds inaweza kuwa lango la amani au vita, Trump achague
Jan 17, 2018 23:03Rais wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina, Mahmoud Abbas amesema mji wa Baitul Muqaddad unaweza kuwa lango la kupatikana amani au kuibua vita, na Marekani ina khiari ya kuchagua njia inayoitaka.