-
HAMAS: Vitisho vya Trump havitutii hofu yoyote
Jan 11, 2025 03:39Mjumbe wa ngazi ya juu wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema: "Vitisho vya Marekani havina umuhimu wowote kwa wananchi wa Palestina. Wapalestina wanajua kwamba wako kwenye haki na wanapigania haki na malengo yao matakatifu ili waweze kuishi katika nchi yao wenyewe kama walivyo watu wa mataifa mengine duniani".
-
Majibu ya nchi mbalimbali kwa madai yasiyo na msingi ya Trump kuhusu kuinyakua Greenland
Jan 09, 2025 12:53Baada ya Rais mteule wa Marekani, Donald Trump kusisitiza madai yake ya kutaka kunyakua maeneo Canada, Panama na Greenland, na hatua zake, ikiwa ni pamoja na kumtuma mtoto wake wa kiume huko Greenland kuandaa mazingira ya unyakuzi huo, nchi hizo zimetoa majibu makali dhidi ya hatua ya Trump.
-
Jaji: Hukumu dhidi ya Trump kutolewa kabla ya kuapishwa kwake
Jan 05, 2025 03:35Jaji wa New York ametangaza kuwa, hukumu dhidi ya Donald Trump Rais mteule wa Marekani itatolewa tarehe 10 ya mwezi huu wa Januari katika kesi yake ya fedha mjini New York siku chache kabla ya kuapishwa kuwa rais.
-
HAMAS yajibu vitisho alivyotoa Trump kuhusu mateka wa Kizayuni wanaoshikiliwa Ghaza
Dec 04, 2024 06:42Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS imetoa jibu kwa ujumbe wa vitisho uliotolewa na rais mteule wa Marekani kuhusu mateka wa Kizayuni wanaoshikiliwa katika Ukanda wa Ghaza na kusisitiza kuwa, ni bora Trump atume salamu zake hizo kwa Netanyahu.
-
Sisitizo la Trump la kuanza duru mpya ya vita vya ushuru katika kipindi cha pili cha urais
Nov 28, 2024 02:51Rais mteule wa Marekani, Donald Trump, ametangaza kuwa katika siku yake ya kwanza akiwa Ikulu ya White House, atatoa agizo la kutozwa ushuru mpya bidhaa zote zinazoagizwa kutoka Mexico, Canada na China.
-
Tahadhari kuhusu matokeo ya kukiukwa haki za binadamu katika kipindi kingine cha urais wa Trump
Nov 11, 2024 10:24Shirika la Human Rights Watch limetoa onyo kali likisema kuwa muhula wa pili wa urais wa Donald Trump ni tishio kubwa kwa haki za binadamu nchini Marekani na duniani kote, na kwamba taasisi huru na jumuiya za kiraia zinapaswa kumuwajibisha rais huyo mpya kuhusiana na suala hili.
-
Sababu zilizopelekea Trump kushinda uchaguzi wa rais wa Marekani
Nov 08, 2024 06:59Hatimaye mchuano mkali uliowaweka watu roho juu, wa kinyang'anyiro cha uchaguzi wa rais wa Marekani wa 2024 uliofanyika Novemba 5, umemalizika na matokeo yake rasmi yametangazwa.
-
Trump amsifu shahidi Luteni Jenerali Qassem Soleimani
Oct 15, 2024 12:12Rais wa zamani wa Marekani na mgombeaji wa uchaguzi ujao wa rais wa nchi hiyo amesema kuwa, Luteni Jenerali Qassem Soleimani aliyeuawa shahidi, kamanda wa zamani wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu cha IRGC, alikuwa jenerali mkubwa sana wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Msaada wa EU kwa Ukraine tangu vilipoanza vita na Russia 2022 umefikia dola bilioni 131
Sep 18, 2024 06:02Misaada iliyotolewa na Umoja wa Ulaya (EU) na nchi wanachama wa umoja huo kwa Ukraine tangu vilipoanza kati ya nchi hiyo na Russia mnamo Februari 2022 imefikia yuro bilioni 118 (dola bilioni 131). Hayo yameelezwa na Makamu wa Rais wa Tume ya EU Valdis Dombrovskis.
-
Mdahalo wa kwanza wa uchaguzi wa rais wa Marekani kati ya Harris na Trump
Sep 12, 2024 07:26Mgombea wa chama cha Demokrat Kamala Harris na mgombea wa chama cha Republican Donald Trump katika uchaguzi wa urais wa Marekani wa Novemba 5, 2024, walishiriki katika mdahalo wao wa kwanza siku ya Jumanne usiku, Septemba 10.