Uganda imejiweka katika hali ya tahadhari kutokana na kuongezeka wasiwasi juu ya uwezekano wa kuenea hadi nchini humo ugonjwa hatari wa Ebola kutoka nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambayo inapambana na mlipuko wa homa hiyo.
Ugonjwa wa Ebola umeua watu wapatao 900 huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) tokea uibuke Agosti mwaka 2018.
Wataalamu wa afya wa Shirika la Afya Duniani WHO wanafanya tathmini kubaini iwapo mripuko wa sasa wa ugonjwa wa Ebola ambao umeua mamia ya watu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo unapaswa kutangazwa kuwa hatari ya kimataifa au la.
Mripuko wa ugonjwa wa ebola umeua zaidi ya watu mia moja katika kipindi cha majuma matatu yaliyopita kwenye maeneo ya kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.
Wizara ya Afya ya Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo imethibitisha kesi nyingine 15 za ugonjwa hatari wa Ebola.
Shirika la Afya Duniani WHO limetoa wito wa kukabiliana na hali ya mlipuko wa homa ya Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC, ambako watu takriban 1,000 wameambukizwa ugonjwa huo.
Kituo cha kutibu Ebola huko Butembo, jimbo la Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC kimehujumiwa na watu wasiojulikana.
Vyanzo mbalimbali ya habari vimeripoti kuwa, wanawake katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wanalazimika kufanya ngono mkabala wa kupewa chanjo ya ugonjwa hatari wa Ebola, ambao umeua mamia ya watu kufikia sasa.
Shirika la Msalaba Mwekundu limesema mamia ya raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo wamekimbilia nchini Uganda baada ya kufanyika uchaguzi mkuu wa Jumapili iliyopita.
Wizara ya Afya ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imetangaza habari ya wagonjwa 24 walioambukizwa ugonjwa hatari wa Ebola kutoroka kituo cha matibabu mjini Beni, mashariki mwa nchi.