Nov 03, 2018 02:56
Uganda imetangaza kuwa Jumatatu ijayo itaanza kutoa chanjo kwa baadhi ya wafanyakazi wake wa huduma ya afya dhidi ya maradhi ya Ebola. Hatua hiyo inachukuliwa kutokana na kuongezeka wasiwasi juu ya uwezekano wa kuenea hadi Uganda homa hiyo ya kuvuja damu inayosababishwa na virusi kutoka nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambayo inapambana na mlipuko wa Ebola.