Sep 14, 2018 03:20
Wizara ya Afya ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo jana ilitoa taarifa mpya na kusema kuwa, wahanga wa ugonjwa hatari wa Ebola wameongezeka tangu mwanzoni mwa mwezi Agosti hadi hivi sasa kiasi kwamba kati ya kesi 133 zilizosajiliwa, 102 zimethibitika kuwa ni za homa ya Ebola.